MAANA YA UTUME
Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma
mwenye kurehemu.
Sifa
njema zote (Himidi) ni za Mwenyezi Mungu pekee, mola wa walimwengu. Na
rehema na amani ziwe juu ya mtume wake Muhammad (s.a.w), na kizazi chake chema
na kilicho twahirika.
Hukumu ya mbinguni na ardhini inapokuwa ni
ya Mwenyezi Mungu mtukufu -pekee- bila ya kuwa na mshirika au mwenye kugombea
cheo hicho, kwa kuzingatia kuwa yeye ndiye Mwenyezi Mungu ambaye hakuna apasaye
kuabudiwa kwa haki isipo kuwa yeye tu, Mfalme mtakasifu mwenye usalama, mtoaji
wa amani, mwenye utawala wa kuyaendesha mambo yote, mtukufu, mwenye nguvu na
ushindi na mwenye utukufu wote na “Yeye ni Mwenyezi Mungu muumba na mwenye
kuvipa vitu maumbile, majina yote mazuri ni yake” na “Yeye ni Mwenyezi Mungu
ambaye hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa yeye, Mjuzi wa mambo ya
ghaibu (yasiyo onekana) na yaonekanayo, Yeye ndiye mwingi wa rehma mwenye
kurehemu”, basi hukumu inapokuwa ni ya Mwenyezi Mungu kwa undani huu na upana
huu na kwa ushahidi wa dalili na maumbile, hakika jukumu la kwanza la hakimu
huyu -kwa upole wake na ukarimu na kwa fadhila yake- ni lazima awawekee viumbe
mambo ambayo yataufanya usalama na utulivu wao ubakie na mambo yenye kuzilinda
haki zao na utukufu wao, na kuzitengeza (kuzitakasa) kabisa tabia zao na
mwenendo wao. Kama ambavyo miongoni mwa majukumu yake ya mwanzo ili kukamilisha
fadhila zake na neema zake na upole wake ni kuwafikishia viumbe wote kwa vizazi
vyao vyote upambanuzi wa sheria zile na hukumu zile, ili manufaa yake
yaweze kuwafikia wote na hoja nayo iweze kutimia kwa viumbe wote.
Na -kwa ufupi- hii ndio mana ya “Utume”
kwa maana yake ya ujumla. Na kutokana na akili ya mwanadamu, kuwa ni yenye
kupanuka na kuendelea, kila zama na karne zinavyo pita, na ikiwa kwenye
maendeleo yenye kupanuka na mwendo wake wa haraka kuelekea kwenye kukomaa na
kuzama na ufahamu ulioenea pande zote, sheria za mbinguni (takatifu) zilikuwa
zikishuka taratibu kulingana na maendeleo ya akili na kupanuka kwake, kiasi
kwamba katika kila zama na kwa kila kaumu sheria zile ziko katika kiwango
kinachowiana na maslahi ya zama zile na watu wale na zenye kulingana na kiwango
cha ukuaji wa fikra wa zama zile na watu wake, zikafikia kileleni (zile sheria)
katika ujumbe wa kiislamu (Kupitia Mtume Mohammad (s.a.w.w)) ambazo alizichagua
Mwenyezi Mungu mtukufu ili ziwe ni sheria bora za mwanadamu katika zama za
kukua kwake kiakili na kufikia kilele cha mwisho na katika zama za
maendeleo yake ya utamaduni wenye kushangaza na ulio mkubwa.
Inshallah tutaendelea kuujadili utume kwa
upana zaidi.
Na ninataraji msaada na msukumo wa Mwenyezi
Mungu.
“Ewe Mola wetu! Hakika sisi tumemsikia
muitaji akiita (watu) kwenye Imani ya kwamba “Muaminini Mola wenu” tuka amini.
(Ewe) Mola wetu! Tusamehe madhambi yetu na utufishe pamoja na watu wema. (Ewe)
Mola wetu! Tupe ulichotuahidi kwa Mitume wako na usituache siku ya kiama (ya
mwisho). Hakika wewe huendi kinyume na ahadi”.
Comments
Post a Comment