MASHIA WALIMU WA AHLUL-SUNNAH WALJAMAA
Imam Maliki anasema, ‘ jicho halijaona wa sikio
halijasikia, wala halijapita wazo katika moyo wa mtu yeyote (kuwa kuna) mbora
kuliko Imam Jaafar Assadiq kwa utukufu, elimu, ibada na ucha Mungu’.
Imam Abu Hanifah anasema, “Lau si miaka miwili, basi
Nuu’man angeangamia” akiwa anakusudia miaka miwili aliyosoma kwa Imam Jaafar
Assadiq (a.s).
Tazama: kitabu Manaqib Ali bin Abi Talib, kuhusu
mazingira ya imam Ja’far As-Sadiq.
Maimamu wa Ahlu-Sunnah wanamsifia na kumwona kuwa ni
mkombozi wao Imam Jaafar As-Sadiq. Je ni nani huyo? Imam Jaafar As-Sadiq ni
Imam wa sita wa waislamu kwa kuteuliwa na Mtume (s.a.w.w), wa kwanza wa maimamu
hao ni Imam Ally na wa mwisho wao ni imamu Mahdi. Hao ndio maimamu wanafuatwa
na Mashia Ithnashariyyah, na kuwaamini kuwa ni maasumu na wasio tenda dhambi na
waliowafanyia uadui ni waovu na waliopupia madaraka yasio kuwa yao.
Comments
Post a Comment