MITUME WOTE WALIKUJA KUWAALIKA WATU
KUMTII MWENYEEZI MUNGU MMOJA.
Mitume wote walioletwa na Mwenyeezi
Mungu walikuja na madhumuni moja, nalo ni kumuongoza mwanaadamu katika njia
moja, nayo ni kumuabudu Mola mmoja. Na Mitume wote walifikia katika kusudio
moja na sio zaidi ya hapo.
Vile vile kulikuwa kuna watu ambao
walikuwa wakikabiliana na Mitume na kuyapinga yale ambayo wanayaamrisha, watu
hao vile vile walisimama kidete kwa kutumia njia moja ili kufikia katika
makusudio yao. (ili kupata ufafanuzi zaidi rejea kitabu cha Elimu ya
Qur-ani, Intisharati simat wa tamhiydiy, ukurasa wa 278).
Lazima tujiulize kama mitume
wote ujumbe wao ulikuwa mmoja, nani sasa kaleta dini nyingi? Au ni nani basi
kaleta madhehebu mengi? Bila shaka hiyo ni kazi ya shetani. Ni lazima tufanya
juhudi za makusudi kuzichunguza dini zetu na madhehebu zetu ili kubaini kama ni
za kweli au za uongo (bandia). Tutakapogundua kuwa dini zetu au madhehebu zetu
ni bandia basi tuzihame mara moja na kuufuata ukweli.
Comments
Post a Comment