MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W) NDIYE WA MWISHO
Sisi Mashia tuna itakidi ya kuwa; Mtume Muhammad
(s.a.w.w) ndiye Mtume wa mwisho wa Mwenyeezi Mungu, na sheria na malinganio
yake ni kwa ajili ya watu wote duniani, na sheria hizo zitabakia milele hadi
mwisho wa dunia, kauli hiyo inathibitisha kuwa taaluma na hukumu zote za dini
ya Kiislamu zinakidhi na kudhamini mahitajio yote ya wanaadamu, ya duniani na
Akhera hadi mwisho wa dunia, kwa hiyo, mtu yeyote yule atakayekuja na madai ya
kuwa yeye ni Mtume, basi madai hayo si ya kweli na yatakuwa hayana msingi
wowote kwa wanaadamu.
Allah anasema katika Qur’an takatifu, “Muhammad
si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Mwisho
wa Manabii, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu”.
Hii ndio itikadi yetu na anayedai kinyume na
hayo dhidi yetu basi ni mwongo anayeeneza imani yake kwa kutuzulia uongo sisi. Hakika
imani inayoenezwa kwa uongo hiyo sio dini sahihi bali itakuwa na ushetani ndani
yake.
Kwa hiyo wale wote wanaotusingizia uongo sisi
Mashia ni mashetani waliojiingiza katika Uislamu ili kuwapotosha waumini. Haiwezekani
wao waujue Ushia (Uislamu) kuliko sisi wenye imani yao.
Comments
Post a Comment