NDOA
Ndoa ni taasisi ambayo iliasisiwa na Allah ‘Azza
wa Jallah
Mwenyewe pale alipowaunganisha baba yetu Adam na mama yetu Hawa kuishi
pamoja kama mume na mke.
Kwa hiyo, Uislamu kama dini na mfumo wa maisha, umeweka kanuni, sheria
na hukumu za kufuatwa ndani ya taasisi hii tukufu (ya ndoa).
Tutakusanya mafundisho yote muhimu yenye kuhusu taasisi hii kutoka
katika vyanzo vikubwa na chimbuko la sheria na mafundisho ya Uislamu, ambavyo
ni Qur’ani na
Sunnah. Nitazileta kwenu ili zimnufaishe kila mtumiaji wa mtandao katika
maisha yake ya ndoa.
Comments
Post a Comment