SHEREHE ZA IDDIL FITRI

SHEREHE ZA IDDIL FITRI
Allah (s.w) anasema “Hakika wabadhirifu ni ndugu zake mashetani; na Shetani ni mwenye kumkufuru Mola wake” (Al-Isra : 27). Ama wakati wa kuimaliza Ramadhani, katika pilika pilika za furaha ya sherehe za Iddi, utajionea mwenyewe namna mwanadamu anavyoghilibiwa kwa haraka na kuchezewa shere na Shetani. Hayo utayashuhudia katika beach, sinema na hata katika tamasha za disco na dansi - na Mungu atuepushe.

Ni kweli kwamba, Mtume (s.a.w.w) alisema, “Mambo mema huyafuta maovu” Lakini papo hapo maovu nayo huyafuta mema.

Sheikh mmoja alipokuwa akisoma darasa msikitini alisema, “Mwenye kulisema neno hili ‘Laahaula Walaa Quwwata Illaa Billahil Adhim’ mara moja tu, Mwenyezi Mungu Humpandia mti wa mtende peponi. Na kila msomapo hupandiwa na hivyo basi kuifanya idadi ya mitende apandiwayo kuwa sawa na idadi ya mara alizosoma.”

“Si mitende hiyo itaijaza pepo hata kukosekana nafasi?” Aliuliza mmoja wa waliokuwepo. Sheikh akamjibu “La, haitajaa maana hata mashoka ya kuikata na kuibwaga chini ni mengi. Kwa mfano: Mtu aliyepandiwa mti huo baadaye atasengenya, au akadanganya, au akafanya kosa lolote lile na kila kosa afanyalo huwa mtende mmoja wabwagwa. Jee! mtu huyo atabakisha kitu?

Na vivyo hivyo sisi lau tutausahau wajibu wetu wa kumtii na kumnyenyekea Mwumba wetu, bila shaka tutakuwa taabani hapo kesho tutakapotiwa adabu." Hakuna faida yoyote ile kwa mtu kushinda mchana kutwa au mwezi mzima akiabudu na kufika usiku au siku ya kufuturu akaasi, maana kufanya hivyo kutakuwa sawa na aliyepeleka Benki Shs. 100,000/- na kabla ya kuzifikisha akazitumia zote. Je, mtu huyo ana kitu alichoweka?
Kesho Jumamosi ni siku ya Idd kwa sisi waislamu. Japokuwa wanafiki wa kiwahhabi wamesherehekea idd siku ya Ijumaa. Katika sherehe hii tuendelee kufanya ibada. Katika siku ya idd na miezi mingine yote ijayo, kwa sababu Ramadhani tunayoimaliza Jumamosi ni chuo cha ucha Mungu na siku ya idd ndio sherehe ya mahafali. Tunapohitimu tunatakiwa tuwe na maarifa na juhudi zote za kutufanya tuendelee kuwa wacha Mungu.

Eid Mubarak 

Comments