SIFA ZA SURA AL-HAMD (AL-FATIHAH)

SIFA ZA SURA AL-HAMD (AL-FATIHAH)
Miongoni mwa Sura za Qur’ani Tukufu, Sura hii inayo hadhi ya juu, ambayo hunyanyuka kutoka kwenye sifa zifuatazo:
1.     Uzito wa Sura hii:
Kimsingi, sura hii inayo tofauti iliyo wazi na sura zingine za Qur’ani Tukufu kutokana na mtazamo wa uthabiti na uzito, kwa sababu sura zingine zote zinatoka kwenye usemi wa Mungu ambapo Sura  hii inatoka kwenye ulimi wa waja.  Na kutoka kwenye Mtazamo mwingine katika Sura hii, Mungu amewafundisha waja wake namna ya kusema na kuwasiliana na Yeye”
          Utangulizi wa Sura hii umeanza na kumsifu na kumtukuza Mola Mlezi.
          Inaendelea na imani mwanzoni na baada ya maisha ya hapa duniani (kumtambua Mungu na imani katika ufufuo), inaisha na mahitaji na masharti ya waja.
         
 Wakati mtu mwenye hadhari, ambaye moyo wake umezinduka anasoma sura hii huhisi kwamba amewekwa kwenye mabawa na manyoya ya malaika, kwamba ananyanyuka kwenda mbinguni, na kwenye uwanja wa kiroho, hatua kwa hatua, anasogea karibu zaidi kwa Mungu (s.w.t.).
          Hili ni wazo bora sana, kwamba Uislamu, katika kukinzana na mifumo mingi ya imani za uongo (ambapo husemekana kwamba wapatanishi wameteuliwa kati ya Mungu na viumbe,) umetangaza kwa wanadamu kwamba bila ya mpatanishi wanatakiwa kuanzisha uhusiano na Muumbaji wao!

          Sura hii ni mfano, ambamo uhusiano huu wa karibu kati ya Mungu na wanadamu imeegemezwa (bila ya wapatanishi), kati ya vilivyoumbwa na Muumbaji.  Mahali hapa yeye (mja) humuona Yeye tu, husema Naye tu, husikiliza ujumbe Wake kwa masikio yake na mwili wake, hivyo kwamba hapana hata Mtume au Mjumbe au mmoja wapo wa Malaika wa karibu sana anakuwa mpatanishi katika uhusiano huu.  Na inastaajabisha kwamba muunganiko huu na uhusiano wa moja kwa moja wa vilivyoumbwa kwa Muumbaji ni mwanzo wa Qur’ani Tukufu.

Comments