SWALA (IBADA) NI NINI?

SWALA (IBADA) NI NINI?
Sala ni matendo na maneno ambayo hujenga mahusiano kati ya Muumba na kiumbe, hivyo mja akiikata, basi mawasiliano yake na Mola wake hukatika.

Allah Mtukufu anasema: “Kwa hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu hakuna aabudiwaye ila Mimi tu, basi niabudu na simamisha Swala kwa kunitaja” (Surat Twaha: 14).

Kila mtu mwenye akili timamu ni lazima atafute utaratibu sahihi wa kuwasiliana na Muumba wake na autumie huo kwa kazi hiyo. Kuna wengine wengine huimba sana na kudai kuwa hiyo ni sala, lakini kwa hakika hizo ni starehe na wala sio ibada. Kuna watu wengi pia huwaabudu wasiokuwa Mwenyezi Mungu, hilo nalo ni kosa kwa sababu wanapoteza nguvu zao bure kwani hivyo wanavyoviabudu havitowafaa kwa lolote.

Hivyo basi tumtambue Mwenyezi Mungu Muumba mbingu, ardhi na kila vilivyomo, huyo ndiye anayestahihili kuabudiwa peke yake.


Comments