SWALI LA KWANZA KWA MAWAHHABI NA MASALAFI
Hitoria inashuhudia kuwa wakati Mtume Muhammad (s.a.w.w)
alipotangaza utume wake, yeye na ukoo wake (Bani Hashim) waliwekewa vikwazo
vikali sana. Waliofanya hivyo ni Maquraish.
Mzee Abu Talib
(as) aliliupeleka ukoo wake katika eneo liitwalo Shib Abi Talib ambapo
alijificha hapo kwa miaka mitatu, wakiteseka kwa njaa kali na shida za kila
aina. Kiasi kwamba walifikia hatua ya kula ngozi za viatu vyao kwa sababu ya
njaa.
Wakati huo Sayyidna Abu Bakar na Umar wakiwa mjini
wakiponda raha. Je huu ndio Uislamu wa watu hawa? Kwa nini hawakumsaidia Mtume
na ukoo wake katika kipindi hiki kigumu? Kama wangeshindwa kujiunga naye
pangoni wangewapelekea walau chakula. Lakini hakuna ushahidi unaoonesha kuwa
waliwapelekea chakula wala nguo. Na kama wangekuwa wakiwapelekea wasingepata
shida kubwa kiasi hicho kwa sababu wote wawili walikuwa na uwezo wa kutosha.
Maquraish ikiwa ni pamoja na Abubakar na Umar
walikutana na kukubaliana kuwa wasifanya biashara yoyote na Bani Hashim na bani
Mutalib na wasioleane na mkataba huo ukaandikwa na kubandikwa ndani ya Alqa’bah,
na wakaahidi kuutekeleza kiukamilifu. Bani Hashim na Bani Mutalib wote
walikwenda kumzunguka mzee Abu Talib (baba wa Imam Ally) katika bonde lake
isipokuwa Abu Lahab aliyejiunga na Maquraish na kushirikiana nao katika vita
vyao dhidi ya Mtume na Ukoo wake.
Rejea:
1. Tarekh Tabari ya kiingereza vol. 6 ukurasa wa 81
2. Siratun Nabi cha Shibli Numani vol. 1 ukurasa wa 218
(tafsiri ya kiingereza ya M. Tayyib Bakhsh Budayuni).
Katika kitabu hiki ameonyesha kuwa walikuwa na njaa
kali kiasi cha kula majani ya miti iliyokuwa hailiwi kabla ya hapo na migomba.
Haya tuelezeni wale mnaodai kuwa walikuwa
marafiki wakubwa wa Mtume walikuwa wapi? Kwa nini hawakumsaidia? Mtu (Abu Talib)
mnayemsingizia kuwa ni kafiri ndiye alikuwa akikesha kumlinda Mtume wakati
waheshimiwa wakistarehe, je huo ndio Uislamu mnaousifia?
Comments
Post a Comment