UTUME (MZIZI WA DINI)

UTUME (MZIZI WA DINI)

Kwa ujumla dini ya Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w), ni dini ile ile waliyokuja nayo Mitume waliopita kabla ya yeye, kuanzia Nabii Nuhu (a.s) mpaka kufikia Nabii wa mwisho Mtume Muhammad (s.a.w), basi Mitume wote ni Mitume wa Mwenyeezi Mungu mmoja, Mola ambaye ndiye mwenye ufalme wa nyumati zote za Mitume hao, vile vile Mitume hao wamekuja na dini moja pamoja na lengo moja, nalo ni kuwaalika wanaadamu wamuabudu Mola mmoja wa haki.

Tutaweza kuyathibitisha hayo kama tutazingatia Aya ya 42-92 ya Suratul-Anbiyaa, aya za sura hiyo zimeelezea kwa uwazi kabisa kuwa Mitume hao walikuwa na lengo moja la kuwaongoza watu katika njia moja, na waumini wote (Waislamu) ni umati mmoja.

Hivyo basi dini zote ambazo ziko nje ya Uislamu zimepatikana kutokana na kazi ya shetani. Ndivyo hivyo hivyo kwa upande wa madhehebu. Kama mungu ni mmoja na Mtume wa mwisho ni mmoja haiingii akilini kuwepo na madhehebu mengi. Inambidi kila mwanadamu afanye uchunguzi wa kina kuhusu usahihi wa madhehebu yake. Kwa sababu nyingi ya madhehebu ni ubatili na matunda ya shetani katika kuwaondoa wanadamu toka kwenye njia iliyonyooka. 

Comments