UTUMWA MAMBO LEO:
Dunia imegubikwa na Utumwa mamboleo unaoendeshwa na
nchi za Magharibi na vibaraka wao. Uendelezaji wa wazi wa aina za utumwa
unaweza kufanikiwa kwa njia ya kusaidia Mipango kama vile “Millenium African Recovery
Plan.” Utandawazi kupitia umiliki wa nguvu za uzalishaji unaofanywa na “Muungano
wa Kimataifa wa Wakiritimba” (Multi National Cartels) tayari upo.
Mfumo huu hupenya kwenye kila tabaka la uchumi wa
dunia, iwe ni bidhaa zinazo zalishwa, kama sukari, silaha za kivita, madawa ya
tiba au biashara ya dhahabu na madini ya platinamu.
Utumwa wa kiuchumi kupitia udhibiti mtiririko wa
mitaji ulimwenguni uko imara mikononi mwa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la
Kimataifa (IMF).
Uharibifu kwa Afrika ulitokea kwa njia ya utawala wa
mabavu wa kikoloni wa moja kwa moja, uliofanywa na Uingereza, Udachi, Ufaransa,
Ureno na Ubeligiji. Hii ilifuatiwa na udhibiti wa nje ya Afrika, kwa kuanzisha
serikali kidhalimu ili kuendelea kudhibiti kwa njia za hila zaidi. Kwa
kufichuliwa vibaraka hawa kwa ajili ya ulimwengu kuwaona, ikawa vigumu zaidi
kuendelea kwa uwazi kusaidia vitendo vyao viovu dhidi ya jamaa zao. Vurugu
zilidhibitiwa ili kuhakikisha kuendelea uingiaji kwenye akiba kubwa za madini.
Njia changamano ilikuwepo kazini kwa zaidi ya miaka
30, ambayo ni kulitumbukiza bara hili (la Afrika) kwenye vita vya wenyewe kwa
wenyewe visivyo na maana yoyote. Ahadi za “kusamehe madeni” zinatolewa kwa
lengo la kuendeleza utumwa kwa Waafrika. Huu “Utumwa Mpya” unaweza kuonekana
tofauti kwa nje na ule wa “West
African Slave Trade” (Biashara ya utumwa ya Afrika ya
Magharibi), lakini misingi yake inafanana.
Kwa kuanzishwa kwa mfumo wa makao makuu ya fedha
(Benki ya Dunia na shirika la Fedha la Kimaraifa), Polisi wa Dunia (North
Atlantic Treaty Organization), imewarahisishia wakoloni kazi ya kuwa na mamlaka
ya kuitawala Afrika.
Mfano wa wazi unaoonyeshwa na nguvu hizi za wakoloni
na washirika wake, ni kuunda taifa la Israeli katikati ya Rasi ya Arabia. Kwa
hiyo ni muhimu sisi kuchambua na kuonyesha ulinganifu huu baina ya Uzayuni
(Zionism) na washirika wake na ukubwa na vipimo vya
utumwa unaoendelezwa na nguvu za wanyonyaji.
Tutaendelea kutoa mada kuhusu kadhia hii ya ukoloni
ili watu wajue namna wanavyotumiwa katika kuwanyonya wao wenyewe na ndugu zao. Ni
vigumu kuelewa mikakati ya maharamia hawa endepo kama usifanya uchunguzi wa
kina.
Utakuta ndugu zetu mawahhabi na masalafi wametumika
sana kuwasaidia wakoloni katika juhudi zao za kuitawala dunia. Utakuta kila
anayeipinga Israel na Ulaya anapigwa vita na Mawahhabi wa Daesh, ISIS, Jabhat
Annusra, Alqaidah na Boko Haramu. Kama kweli wao wanapambana na utumwa na
umagharibi kama wanavyosema kwa midomo basi wangeenda kupambana nao nchini kwao
badala ya kuwauwa waislamu katika nchi zao wenyewe au kusafirisha magaidi
kutoka ulaya na kuwapeleka mashariki ya kati kuwalipua watu.
Comments
Post a Comment