WAISLAMU WAAGIZWA KUISHI VYEMA NA WATU WA DINI
NYINGINE
Ingawaje sisi Waislamu tuna itakidi ya kuwa dini
ya Kiislamu ndiyo dini pekee iliyo rasmi katika zama hizi tulizonazo, lakini
vile vile tunaamini ya kuwa ni lazima tuishi kwa salama na amani na wafuasi wa
dini nyengine, inawezekana wafuasi hao wakawa wanaishi katika nchi za Kiislamu,
au pia wakawa hawaishi katika nchi za Kiislamu, isipokuwa kwa wale wanaopinga
na kupiga vita dini ya Kiislamu.
Allah (s.w)
anasema katika Qur,an kuwa Mwenyezi Mungu hakukatazeni kuwafanyia wema na
uadilifu wale ambao hawakukupigeni vita, wala hawakukutoeni makwenu. Hakika
Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao uadilifu (Surat Mumtahinah Aya ya 8).
Sisi tunaamini ya kuwa; ikiwa dini ya Kiislamu
itaarifishwa kimantiki, basi kutakuwa na uwezekano wa kuibainisha kwa uwazi
dini hiyo kwa watu wote duniani, na kwa sababu dini ya Kiislamu ina dalili zenye
nguvu na zinazokubalika kiakili na kimantiki basi kuna uwezekano wa kuwaongoa
watu wengi duniani, katika dunia ya leo watu wengi wana kiu ya kusikia ujumbe
wa dini ya Kiislamu.
Hivyo basi Uislamu ni dhahabu inayotafutwa na
kila mtu, kinachofanywa na Mawahhabi kuwaua watu kwa madai kuwa sio waislamu au
kwamba ni watu wa bid’a ni ukafiri waliokubuhu na usiokubalika ndani ya
Uislamu.
Comments
Post a Comment