ITIKADI YA WAISLAMU KUHUSU TAUHIID.
Umma
wa Kiislamu tangu mwanzoni umeshikamana juu ya Tauhudi katika nyanja zake mbali
mbali, ukaafikiana juu ya kuipwekesha dhati ya Mwenyezi Mungu na kwamba, yeye
ni mmoja hana mshirika wake na ni mpweke hana mfano.
Kama
ambavyo umeafikiana ya kwamba, yeye ni Muumba na hapana muumba asiyekuwa yeye.
Amesema
Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Je, kuna muumba asiyekuwa Mwenyezi Mungu"
Qur'an, 35:3
Na
Amesema tena:
"Waambie,
Mwenyezi Mungu ndiye muumba wa kila kitu"
Qur'an, 13:16.
Vile
vile umekubaliana juu ya Tauhidi yake katika Rububiya yake na kwamba hapana
Mola wala mwenye kusimamiya (mambo yao) asiyekuwa yeye.
Amesema
Mwenyezi Mungu:
Yeye
ndiye anayesimamia mambo yote hakuna muombezi ila baada ya idhini yake, huyo
ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu basi muabuduni yeye, Je, hamna kumbukumbu?
Pia
wamekubaliana kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika Ibada na kwamba, yeye Mwenyezi
Mungu ndiye Mola ambaye anastahiki kuabudiwa na hukuna wa kuabudiwa asiyekuwa
Yeye.
Mwenyezi
Mungu Amesema:
"Waambie,
Enyi mliopewa Kitabu, njooni kwenye neno lililo sawa kati yetu na ninyi ya
kwamba, tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, na wala tusimshirikishe na
chochote, wala baadhi yetu tusiwafanye kuwa waungu badala ya Mwenyezi
Mungu".
Qur 'an, 3:64
Bali
hizi ndizo nukta ambazo zenye kuafikiana baina ya sheria zote za mbinguni, na
yote haya yanaonekana kuwa ni miongoni mwa mambo ya kipekee kwa baadhi ya
wafuasi wa sheria zilizopita. Basi mtazamo ulio kinyume na misingi hii ni
miongoni mwa vitendo vya uchafuzi na kupotosha vinavyotokana na wanachuoni,
Watawa na Makasisi (wao).
Amma Mawahhabi, Masalafi na Answar Sunnah wana msimamo tofauti na
huu. Katika juhudi zao na upotevu wao wamepotoka katika kumtambua Muumba na
kumsifia kwa sifa asizokuwa nazo na pia kumpunguzia sifa zake. Itakujia mada
mahsusi katika kadhia hii ya Mawahhabi.
Comments
Post a Comment