MAWAHHABI NA
MASALAFI WAMTUKANA MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W).
Watu hawa
waliobobea kwa unafiki wamekuwa wakimtangaza Mtume wetu kuwa hukosea lakini
wakidai kuwa masahaba hawakosei.
Mfano wa
matusi yao kwa Mtume (s.a.w.w) ni pale wanapotafsiri aya ya surat Abasa yaani
sura ya 80 humtuhumu Mtume kwa kudharau watu na kushindwa kutekeleza ujumbe wa
Allah kwa ufasaha ili tu kuwalinda viongozi wao ambao ndio waliolengwa na aya
za mwanzo katika surah hiyo.
Aya ya
kwanza na ya pili zinasema kuwa alikunja uso na akageuka kwa sababu alijiwa na
kipofu. Kosa hili wanamtupia Mtume ili kuwalinda viongozi wao.
Imepokelewa
toka kwa mama wa waumini bi Aisha bint Abubakar (r.a) kuwa siku moja Mtume
alikuwa katika kikao na wakubwa wa kikuraishi akiwamo: Abujahli bin Hisham,
Utba bin Rabia akiwaita katika dini ya Allah. Mara akaja Abdullah bin Ummi
Makhtum, ambapo Mtume ameshughulika na Maquraishi. Abdullah akamuuliza Mtume.
Mtume akakunja uso na akageuka. Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha aya ya 1 na 2.
Hii ndio imani ya mawahhabi.
Tazama:
Addurul
Manthur J6 uk. 517
Tafsirul Qurtubi
J19 uk 211
Tafsir Ibn
Kathir J4 uk 502
Ona ajabu ya
watu hawa wanakubali uongo huu unaohadithiwa kwa kutumia jina la Aisha ambaye
alikuwa hajazaliwa. Kwa sababu imeteremkia Makkah. Kipindi hiki aidha Aisha
alikuwa hajazaliwa au alikuwa mdogo sana kuweza kuhadithia tukio zito kama
hili.
Lakini waislamu
wa kweli (Mashia) tunaamini kuwa Mitume ni maasumu (hawafanyi dhambi). Tendo la
kudharau kipofu sio miongoni mwa sifa za mitume. Ikumbukwe kuwa Allah anamsifia
Mtume wake akisema kuwa ni kilele cha tabia njema (Surat Qalam).
Ukweli ni
kuwa aliyekunja uso ni Uthuman bin Afan na ndiye aliyelengwa na aya hizo ili
kumwonya asifanye tabia mbaya kwa kipofu tena mbele ya Mtume (s.a.ww.).
Ushahidi:
Tafsir Basair
J.52 uk. 230
Tafsir Saafi
J.5 uk. 284.
Almizan Fitafsiril
Qur’an j.20 uk. 308
Majmaul Bayani
Fitafsiril Qur’an J.5 uk. 437
Alburhan
fitafsiril Qur’an J.4 uk. 427
Comments
Post a Comment