MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W)

MTUME MUHAMMAD (S.A.W.W)
Qur’an Tukufu inamtaja Mtume Muhammad (s.a.w.), kama ifuatavyo:
“Bila shaka amekufikieni Mtume kutoka miongoni mwenu, yanamhuzunisha yanayokutabisheni, anakuhangaikieni, kwa waumini ni mpole, mwenye kurehemu.”(9:128)
“Nasi hatukukutuma ila uwe rehema kwa walimwengu.” (21:107)
Huyu ndiye Mtume aliyeweza kufanya mabadiliko makubwa duniani kuliko mtu mwingine yeyote. Wasiokuwa waislamu wanasema yafuatayo kuhusu mtu huyu:

 “Nimeumchunguza yeye (Mohammad). Ni umtu anayevutia ajabu; na kwa maoni yangu, mbali na kuwa mpinga Kristo, ni lazima aitwe mwokozi wa wanadamu.”

“Nina amini kwamba endapo mtu kama huyo angeshika udikteta wa ulimwengu wa kisasa, ange fanikiwa katika kutatua matatizo yake katika namna ambayo ingeuletea ile amani na furaha inayohitajika hasa”

“Kama dini yoyote ingekuwa na fursa ya kutawala uingireza, hasha, bali Ulaya nzima katika kipindi cha miaka 100 ijayo, itakuwa ni Uislamu.”

“Siku zote nimeichukulia dini ya Mohammad katika hadhi ya hali ya juu kwa sababu ya changamoto zake za ajabu. Ndiyo dini pekee ambayo kwangu mimi ninaiona kuwa na uwezo wakuwiana na mabadiliko ya kila zama za maisha ambayo inaweza kuvutia katika kila zama.”
George Barnard Shaw katika “The Genuine Islam” Juz. 11 na. 8 (1936)


Ni maelezo mafupi ya wasifu wa Mtukufu Mtume wa Mungu mwenye nguvu sana, Muhammad (s.a.w.), ambaye kuhusu yeye Qur’an Tukufu inasema:
“Bila shaka amekufikieni Mtume kutoka miongoni mwenu, yanamhuzunisha yanayokutabisheni, anakuhangaikieni, kwa waumini ni mpole, mwenye kurehemu.”(9:128)
“Nasi hatukukutuma ila uwe rehema kwa walimwengu.” (21:107)

Huyo ndiye mwokozi wa ulimwengu huu, nakuombeni tumwitikie katika wito wake na tuwe waislamu wa kweli na wapenda amani kama alivyokuwa yeye. Na wala tusiugeuze uislamu kuwa uwanja wa vita na karaha kwa wengine kiasi kwamba ionekane kuwa kukaa na mwislamu ni balaa. 

Comments