SIFA ZA SHI’A

SIFA ZA SHI’A
Halikadhalika, Abu’l-Muwayyid Muwafiq Bin Ahmad Khawarizmi katika sura ya 17 ya Manaqib yake; Hakim Abu’l-Qasim Abdullah Bin Abdullahi’l-Haskani, katika Shawahidu’t-Tanzil; Muhammad Bin Yusuf Ganji Shafi’i katika Kifayatu’t-Talib, uk. 119, Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkira, uk. 31, Munzir Bin Muhammad Bin Munzir, na hususan Hakim, wamesimulia kwamba Hakim Abu Abdullah Hafidh (mmoja wa maulamaa wakubwa wa kisunni) alisema, akitegemea juu ya ushahidi wa wasimuliaji kurudi nyuma hadi kufikia kwa Yazid Bin Sharafi’l-Ansari, mwandishi wa Amiru’l-Mu’minin Ali Bin Abi Talib kwamba:

Imam  Ali alisema kwamba wakati wa kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), Mtume aliegema kwenye kifua cha Ali na akasema: “umeisikia ile aya tukufu: ‘Wale ambao wameamini na wakafanya matendo mema, hao ndio bora wa viumbe.’ (98:7)
Hawa ni Shi’a wako. Sehemu yangu ya kukutania na wewe itakuwa ni kwenye Chemchemu ya Kauthar (katika Pepo). Wakati viumbe wote watakapokusanyika kwa ajili ya hesabu, uso wako utang’ara, na utatambulishwa siku hiyo kama kiongozi wa watu wenye nyuso angavu.”
Jalalud-Din Suyuti katika Durru’l-Mansur anamnukuu Abu’l-Qasim Ali Bin Hasan (anayejulikana zaidi kama Ibn Asakir Damishqi) ambaye anamnukuu Jabir Bin Abdullah Ansari, mmoja wa masahaba wakubwa wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), akisema kwamba yeye na watu wengine walikuwa wamekaa pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wakati Ali Bin Abi Talib alipoingia ndani. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: “Naapa kwa Yule ambaye anamiliki uhai wangu kwamba mtu huyu (Ali) na wafuasi wake watapata wokovu katika Siku ya Ufufuo.” Wakati huo huo aya hiyo hapo juu ilishushwa.
Katika sharhe hiyo hiyo, Ibn Adi anamnukuu Ibn Abbas akisema kwamba wakati aya hiyo hapo juu iliposhuka, Mtume akasema kumuambia Amiru’l-Mu’minin, Ali: “Wewe na waafuasi wako mtakuja Siku ya Ufufuo katika hali ambayo kwamba wote mtaridhia juu ya Allah, na Allah ataridhika nanyi.”

Katika Manaqib ya Khawrizmi, ifuatayo ilisimuliwa kutoka kwa Jabir Bin Abdullah Ansari: “Nilikuwa kwenye hadhara ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wakati Ali alipoungana nasi, na wakati ule Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: ‘Huyu ambaye amekujieni ni ndugu yangu.’
Kisha, akaelekea Ka’ba, Mtume akachukua mkono wa Ali na akasema: “Naapa kwa Yule ambaye anamiliki uhai wangu, huyu Ali na (Mashia) wafuasi wake watakuwa wamepata wokovu katika Siku ya Hukumu.’

Kisha akasema: ‘Ali ndiye wa mbele zaidi yenu wote katika imani, mwenye kuzingatia mno kuhusu dhamana za Allah, mwadilifu kupita wote katika kuamua mambo ya watu, na mwadilifu kupita wote katika kugawa masurufu miongoni mwa watu, na aliye juu zaidi ya wote kwa cheo mbele ya Allah.’” Katika wakati huo aya hiyo hapo juu ilishushwa.

Katika Sura ya 11 ya Kitabu chake “Sawa’iq” Ibn Hajar anamnukuu Hafidh Jamalu’d-Din Muhammad Bin Yusuf Zarandi Madani (Mwanachuo mkubwa wa Ahlul Sunnah) akisema kwamba: Wakati Aya hiyo hapo juu ilipoteremshwa, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: “Ewe Ali, Wewe na Shi’a wako ndio wabora wa viumbe walioumbwa.
Wewe na Mashi’a wako mtakuja Siku ya Hukumu katika hali ambayo nyote mkiwa mmeridhia kwa Allah, na Allah atakuwa radhi nanyi. Maadui zako watakuwa wamechukizwa mno, na mikono yao itakuwa imefugwa kuzunguuka shingo zao.” Kisha Ali akauliza, ni nani maadui zangu. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akajibu, “Yule ambaye ana uadui kwako na ambaye anakutukana.”

Allama Samhudi, katika Jawahiru’l-Iqdain, kwa idhini ya Hafidh Jamalu’d-Din Zarandi Madani na Nuru’d-Din Ali bin Muhammad bin Ahmad Maliki Makki, ajulikanaye kama Ibn Sabbagh, ambaye anaheshimiwa kama mmoja wa Wanachuo Mashuhuri wa kisunni na mnadharia mkubwa wa mambo ya dini, katika kitabu chake “Fusulu’l-Muhimma” anasimulia kutoka kwa Abdullah bin Abbas, kwamba wakati Aya hii iliyo kwenye mjadala ilipoteremshwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema kumuambia Ali; “Ni wewe na Mashi’a wako. Wewe na wao mtakuja Siku ya Hukumu mkiwa mmefurahi mno na mmeridhia, ambapo maadui zako watakuja na huzuni kubwa na mikono iliyofungwa.”
Mir Seyyed Ali Hamadani Shafi’i, mmoja wa wanachuo wenu mashuhuri katika kitabu chake “Mawaddatul’l-Qurba” na mwanachuo anayejulikana vizuri sana kwa upinzani wake juu ya Shia, Ibn Hajar katika kitabu chake “Sawa’iq-e-Muhriqa”, anasimulia kutoka Ummu’l- Muminina Umm Salma, mke wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), kwamba Mtume alisema:
Ewe Ali, wewe na Mashia wako mtaishi Peponi; wewe na Mashia wako mtaishi katika Pepo.” Mwanachuo anayejulikana sana wa Khawarizm, Muwaffaq bin Ahmad, katika kitabu chake “Manaqib” Sura ya 19, anasimulia kutoka rejea zinazoaminika kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema kumuambia Ali: “Katika umma wangu wewe ni kama Masihi Isa Mwana wa Mariamu.”

Taarifa hii inaonyesha kwamba, kama vile wafuasi wa Mtume Isa (A.S.) walivyogawanyika katika makundi: Waumini wa kweli wajulikanao kama Hawari’in, Mayahudi, na wapiga chuku (wenye kutia maneno chumvi) ambao wanamshirikisha yeye na Allah; katika njia hiyo hiyo Waislamu watakuja kugawanyika katika makundi matatu. Mojawapo litakuwa Shi’a, waumini wa kweli. Kundi lingine litakuwa la maadui wa Ali, na kundi la tatu litakuwa la wenye kukuza cheo chake.

Alhamdulillah, mimi ni miongoni mwa Mashia wa Imam Ally (a.s). Nawaomba maadui wake watubu na wajiunge nasi katika Uislamu sahihi. 

Comments