ALAMA ZA BALEGHE KWA MWANAMKE

ALAMA ZA BALEGHE KWA MWANAMKE
Kuna baadhi ya watu ambao wanaweza kupitiwa na miezi kadhaa tangu kubaleghe, hali ya kuwa hawalijuwi suala hili muhimu. Na kwa wakati huo utekelezaji wa wajibu wa  mambo ya kisharia utakuwa umempita katika kipindi hicho. Hakika utambuzi wa jambo hili unahitaji kuwa makini kwa namna Fulani, japokuwa ni jambo jepesi kwa upande wa wasichana kwani lina uhusiano na alama tatu ambazo moja miongoni mwa hizo inatosha kuwa dalili ya kubaleghe. Alama hizo ni hizi zifuatazo:-
1-Umri
Nao ni kutimiza miaka tisa ya mwaka unaofuata kalenda ya mwezi mwandamo. Mwaka wa kalenda ya mwezi mwandamo ni pungufu kwa siku kumi na saa kumi na nane ukilinganisha na mwaka unaofuata kalenda ya Jua wa mawiyo (Grigorian callender).
2- Nywele ngumu za Sehemu ya Siri:
Hizi ni nywele zinazodhihiri chini ya tumbo.
3- Damu ya Mwezi:

Miongoni mwa alama za kubaleghe, ni kupata damu ya mwezi (yaani hedhi). Na mara nyingine hupatikana alama nyingine kama vile kuongezeka kimo, kuota matiti na kupanuka kwa uke.

Comments