CHEO CHA SALMAN, ABU DHARR,
MIKDADI NA AMMAR (R.A)
Assalaam alaykum:
Masunni husimulia Hadith kutoka
kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) isemayo: “Hakika masahaba wangu ni kama nyota;
yeyote katika wao mtakayemfuata, mtakuwa mmeongozwa sawa sawa.
Abu’l-Fida anaandika katika
kitabu chake cha Tarikh kwamba watu hawa wanne, ambao walikuwa masahaba wa
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) walijitenga, pamoja na Ali kula kiapo cha utii kwa Abu
Bakar, siku ile ya Saqifa. Bila shaka kitendo cha masahaba hawa ni cha kuigwa
na sisi Mashia tunawaiga wao kuupinga utawala wa Abubakar bin Quhafa.
Maulamaa wa Kisunni wameandika
kwamba watu hawa wanne walipendwa na Allah na Mtume Wake. Sisi tunawafuata kama
walivyomfuata Ali.
Abu Nu’aim Isfahami katika
“Hilyatu’l-Auliya”, Juz. 1, uk. 172 na Ibn Hajar Makki katika hadith ya tano ya
hadith arobaini zilizosimuliwa katika “Sawa’iqul- Muhriqa” kwa kumtukuza Ali,
iliyosimuliwa kutoka kwa Tirmidhi, na Hakim kutoka kwa Buraida, kwamba Mtukufu
Mtume (s.a.w.w.)) alisema: “Hakika, Allah ameniamuru mimi kuwapenda watu wanne
na amenijulisha kwamba Yeye mwenyewe anawapenda.”
Wakati watu walipomuuliza ni
kina nani watu hao wanne, alisema: “AIi ibn Abu Talib, Abu Dharr, Mikdadi na
Salman.”
Tena, Ibn Hajar katika Hadithi
ya 39 amesimulia kutoka kwa Tirmidhi na Hakim kutoka kwa Anas bin Malik kwamba
Mtume amesema: “Pepo inashauku juu ya watu watatu, Ali, Ammar, na Salman.”
Je, vitendo vya Sahaba hawa
Mashuhuri wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) sio vya mfano wa kuigwa na Waislamu
wengine? Je, sio aibu kwamba kwa maoni ya masunni Sahaba wamewekewa mpaka kwa
wale tu waliocheza mchezo wa Saqifa, au ambao wameukubali mpango wake bila kupinga,
ambapo wengine ambao wamepinga hila za Saqifa wanaonekana kama wasiokuwa
waaminifu?
Hakika Masahaba hawa walikuwa
wachamungu wasio tiliwa shaka hata kidogo. Na hao ni mfano mwema kwetu sisi
Mashia. Hatutaki kuona dhuluma wala kwenda kinyume na maelekezo ya Allah na
Mtume wake hata kidogo.
Comments
Post a Comment