DINI NI NINI?
Neno hili lenye asili ya Kiarabu, “Diin” (دین) linatumika kwa maana nyingi kidogo.
1. “Uislamu; imani ya Umoja wa Mwenyezi Mungu;
Ibada; Utii; Matendo yote ya kiibada na Ucha Mungu.” Maana zote hizi
zinahusiana zenyewe kwa zenyewe na zahusika na imani ya kuwepo Muumba.
2. “Hukumu; Thawabu au Adhabu; Hesabu Amri;
Sheria.” Maana hizi, nazo pia, zahusiana zenyewe kwa zenyewe na zatushabihisha kwenye imani ya Maisha ya
Akhera.
3. Kikundi cha tatu cha maana ya neno hili ni
“Desturi; Tabia; Mazoea; Aina zote mbili za Dini iliyoteremshwa na Mwenyezi
Mungu au ya kimapokeo kutokana na wahenga.” Maana hasa ya neno hili Diin (دین) ni kuwa mwanadamu kwa silika zake za asili, hana budi kuwa na
mpango wa maisha wenye msingi wa fikara za kiroho au fikara zile tuziitwazo
“Imani”.
Hivyo basi, inaonekana kuwa, neno (دین) lina maana kubwa mno kuliko ile ya neno la Kiingereza
“Religion”, ambayo husisitiza maana ya Mwanadamu kuitambua Nguvu kubwa kuliko
yeye, na ambayo inautawala ulimwengu mzima, na hasa Mungu au miungu ya mtu
kibinafsi, ipasikayo kutiiwa na kuabudiwa; matokeo ya utambuzi wa aina hiyo;
mwongozo wa kiroho wa mtu; au mpango maalum wa Kiimani na kiibada.
Comments
Post a Comment