FAIDA
ZA KUUSOMA UISLAMU
Sifa
zote njema ni za Mwenyezi Mungu Mtukufu, na rehema na amani zimshukie Mtume
Wake Muhammad (SAW), Nabii wa Mwisho, na juu ya kizazi chake kitakatifu.
Hakika
Umma wa Kiislamu umeshindwa kabisa, na kushindwa huko kunafuatia machungu na
mateso; kisha ukosefu mkubwa katika pande mbili: upande wa kimaada (kidunia) na
upande wa kimaanawi (kiroho). Kukosekana upande wa kimaanawi ni sababu ya
kukosekana upande wa kimaada, kwani umaada sio nguvu inayojileta yenyewe kwa
mtu na kuweza kubaki au kuondoka wakati wowote, bali ni natija ya kazi ya mtu
na mapato ya juhudi yake. Mtu hafanyi bidii ila baada ya kujua maana ya juhudi
yake.
Kwa
hivyo, kukosekana umaanawi katika Umma wa Kiislamu ndiko ambako kunapasa
kuupiga vita na kuupigania ili urudi utukufu na ushindi na Umma uishi katika
neema baada ya kuwa katika adhabu. Hatuwezi kuupiga vita ukosefu huu bila ya
kueneza mwamko sahihi wa Kiislamu kwa kutafsiri Qur'ani, kueneza maarifa yake. Kuelezea
maisha ya mashujaa wa Kiislamu.
Hii ndio sababu
iliyonifanya nitumia muda wangu kuandaa mada mbali mbali na kuziingiza katika
mtandao ili ndugu zangu waislamu na wale wasiokuwa waislamu wasome na waelewe
maanawiya ya kiislamu. Uislamu ukieleweka vizuri, tutapata maendeleo na nchi
yetu itakuwa na amani tele.
Comments
Post a Comment