HISTORIA YA CHANZO CHA
MAWAHHABI
Mwenyezi Mungu Mwenye Rehma
amesema katika Qur’ani tukufu kuwa: “Akasema: Hakika wafalme wanapouingia
mji, wanauharibu na wanawafanya watukufu
wake kuwa dhalili; hivyo ndivyo wanavyofanya”. (27:34)
Aya hii inatoa ujumbe kwa
Waislamu ulio muhimu sana. Inaeleza kwamba unapotokea ufalme usiotosheka na milki yake na ukawa na nia ya kutaka
kupanua himaya yake na mipaka yake, basi
daima ufalme kama huu hauwezi kuzingatia kanuni za haki katika nidhamu yake. Na hapo ufalme huo hupotoka na
kuanza kuvamia nchi nyingine na kuiteka miji yake na kufanya ufisadi ikiwa ni
pamoja na kuharibu mali na kuhilikisha maisha ya wanadamu. Kwa kuwa Mawahhabi historia yao inaonyesha kutokana
kwao na mambo ya ufalme na mauaji hapana
shaka kuwa aya hii inazungumzika katika fitna yao.
Comments
Post a Comment