MAANA YA MAWAHHABIYA
Kwa kufuatana na maelezo ya
wanachuoni waliochimbua Historia ya Wahhabi, neno “Wahhabi” limetokana na jina
la Abdul Wahhab ambalo ni jina la baba wa Sheikh Muhammad bin Abdul Wahhab.
Wale watu wanaofuata itikadi
potofu ya Sheikh Muhammad ndio hao wanaoitwa
“Wahhabi”. Wanachuoni wengi walichagua wafuasi hawa wa itikadi potofu
waitwe kwa lakabu hiyo kwa sababu wanaona kwamba isingewezekana kuitwa “Muhammadiya”
sawa na jina la Sheikh wao kwa kuwa jina hilo ni la Mtukufu Mtume
(s.a.w.). Isingekuwa vyema watu wapotofu
na mafisadi kama hawa wanaopotosha mafuzo yake wachukue jina lake kuwa anuani
ya uharibifu wao. Na vile vile mara nyingi
wanachuoni hujulikana kwa lakabu zao. Mfano ni huu: Ibn Jauz, Ibn Nabati, Ibn Kathiir, Ibn
Jarir, Ibn Maja, Ibn Sina, Ibn Qayyim, Ibn Askary n.k. Na yeye Sheikh Muhammad
akaitwa Ibn Abdul Wahhab.
Comments
Post a Comment