MWANZO WA WAHYI (UFUNUO AU REVELATION)
Amesema Bukhari na Muslim na wengineo kuwa: Imepokewa kutoka kwa Azzuhry naye amepokea kwa U'rwa bin Zubeir naye amepokea kwa Mwana Aisha (mkewe Mtume) kwamba: Malaika Jibril (a.s) alikuja kwa Mtume (s.a.w.) naye akiwa katika pango la Hiraa akamwambia: Soma.
Amesema Bukhari na Muslim na wengineo kuwa: Imepokewa kutoka kwa Azzuhry naye amepokea kwa U'rwa bin Zubeir naye amepokea kwa Mwana Aisha (mkewe Mtume) kwamba: Malaika Jibril (a.s) alikuja kwa Mtume (s.a.w.) naye akiwa katika pango la Hiraa akamwambia: Soma.
Mtume akajibu: Mimi sijui kusoma. Mtume
anasema: Malaika akanikaba kwa nguvu mpaka nikazidiwa kisha akaniambia: Soma,
Mtume akajibu: Mimi sijui kusoma. Kisha ndipo Malaika alipomsisitiza kwa nguvu
akisema: "Soma kwa jina la Mola wako, ambaye ameumba. Amemuumba mwanadamu
kutokana na damu iliyoganda. Soma na Mola wako ni Mtukufu kuliko wote". (Qur'an,
96:1-3).
Baada ya hapo, Mtume (s.a.w.) alirudi kwa mkewe
mwana Khadija (a.s.) akiwa amejawa khofu kubwa. Alipoingia ndani alijitupa
chini na huku akilalamika: "Nifunikeni, nifunikeni!!" Alipotulia
akasema: "Ninaogopa sijui kitanipata nini?!" Khadija akamtuliza:
"Sivyo! Wallahi Mwenyeezi Mungu hatakuangamiza abadani, wewe unaunga
udugu, unavumilia matatizo, unasaidia wanyonge, unasaidia kuleta haki."
Kisha Khadija akamchukua Mtume akampeleka kwa
Ibnu ammi yake Waraqa bin Nawfal (alikuwa mnasara, mwandishi wa Injili kwa
lugha ya kiibrania). Walipofika kwa Waraqa, Khadija akamwambia: "Ewe Ibnu
ammi! Msikilize Muhammad aliyo nayo." Waraqa akamuuliza, "una nini?"
Muhammad akamwelezea yote kama aliyoyaona, Waraqa akamwambia: "Huyu ni
Malaika ambaye amepata kumteremkia vilevile Nabii Musa (a.s.) Ee!!!"
Natamani kama nitakuwa hai wakati watakapokufukuza watu wako!!! Muhammad
(s.a.w) akashituka: "Watanifukuza??" Waraqa akajibu: "Ndiyo, hakuna
mtu yeyote anayeleta jambo kama hili uliloleta wewe isipokuwa atapigwa vita na
watu wake".
Tazama:
Sahihi Bukhari J.I uk, 5-6
Sahihi Muslim J. I uk, 97
Almuswannaf J. 5 uk, 322
Tarikhut Tabari J. 2 uk,
47
Ebu tujadili kidogo. Je
hadith hizi ziko sahihi? La hasha haziko sahihi. Hadith hizi ziliandikwa na
maadui wa Mtume yaani Bani Umaya ili kumdhalilisha Mtume wetu, kwa sababu
zifuatazo.
1. Suala la kumtaalifu mtu kuwa ni mtume hufanywa
na Mungu mwenyewe kupitia kwa malaika Jibrail na si vinginevyo.
2. Ukweli hauwezi kutambulika kwa kupitia upotofu,
mnaswara ni mtu aliyepotea njia kwa sababu wao wanaamini kuwa Yesu ni Mungu au
mwana wa Mungu, haiwezekani alete hoja kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah.
3. Hadith hii imetumika na wakristo kuudhalilisha
Uislamu kwa maana kuwa aidha Muhammad alipewa utume na Khadija au kasisi wa
kikristo kwa maana kuwa Mtume wetu alikuwa mtumishi wa kanisa. Allah hawezi
kuacha mwanya wa namna hii.
4. Muhammad (s.a.w.w) alijulikana kuwa ni Mtume
tokea alipokuwa motto, haiwezekani ajisahau cheo pindi alipokuwa mkubwa hadi
akaambie cheo chake ni wakristo.
5. Suala la kusoma, Mwenyezi Mungu anasema
kumwambia Mtume, “Tutakufundisha na wala hautosahau”. Suala la kumfundisha
Mtume halikuwa la kupigana tena kama shule zetu, bali Allah alimfundisha
kimuujiza. Kwani inajulikana kuwa ufundishaji wa kawaida watu husahau.
6. Ilikuwa ni desturi ya wayahudi na wakristo
kubuni hadith na kuzipachika katika vitabu vyetu, ni lazima tuwe makini katika
kukubali hadith kwa sababu zingine zinakwenda kinyume na Uislamu. Waliagizwa na
watawala wa zama hizo kufanya hivyo kwa maslahi ya watawala waliojiita kuwa ni
makhalifa.
Nitaleta hadith sahihi
kuhusu suala hili, kunako majaliwa ya Mola.
Comments
Post a Comment