NAMNA YA KUTAWADHA

NAMNA YA KUTAWADHA
Kabla ya kuswali ni lazima utawadhe {ufanye Wudhu}.
Na namna ya kutawadha ni kama ifuatavyo:-
{a} Chukua maji mataharifu na ya halali, na viwe viungo vyako ni tohara.
{b} Kosha mikono yako viganjani mara tatu.
{c} Sukutuwa na utie maji puwani, kila kimoja mara tatu.
{d} Kisha kusudia kuwa "Mimi ninatawadha kwa kutaka ukaribu wa Mungu.
{e} Osha usoni kwako, kuanzia maoteo ya nywele za kichwa. na utakosha mpaka kidevuni, ndio urefu na ukati wa dole gumba na kidole cha shahada, ndio upana wa uso.

{f} Baadae utakosha mkono wa kulia, kuanzia juu ya kisigino, mpaka nchani mwa vidole.
{g}Kisha utaosha mkono wa kushoto vilevile.

{h} Kisha utapaka kwa kiganja chako cha kulia sehemu ya mbele ya kichwa.
{i}Baadae utapaka kwa mkono wako wa kulia juu ya mgongo wa unyayo wako wa kulia, kuanzia vidoleni mpaka katika kifundo.
{j} Baadae utapaka kwa mkono wako wa kushoto juu ya mgongo wa unyayo wa kushoto vilevile.

Hapo udhu tayari na unakuwa tayari kwa ibada. Utaratibu huu ni kwa mujibu wa Qur’an na sunnah za Mtume Muhammad (s.a.w.w). Tofauti na hivi ni utaratibu uliobuniwa baadaye na watawala waliowatawala waislamu kwa mabavu na ninaweza kudiriki kusema kuwa ni bid’a.


Hala hala, tunapoipata Sunnah moja tuitekeleze mara moja na tunaifahamu bid’a moja tuachane nayo mara moja hata kama tumezoea kuifanya, insha-Allah.

Comments