SIFA BORA ZA SHIA ZATHIBITISHWA
KUTOKA KWENYE VITABU VYA KISUNNI.
Katika kitabu kiitwacho
Mawaddatu’l-Qurba amenukuliwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akisema, “Ewe Ali, Siku
ya Hukumu wewe na Mashi’a wako mtakuja mbele za Allah mkiwa mmefurahi mno na
kuridhia, ambapo adui yako atakuja na huzuni kubwa na mikono ikiwa imefungwa.”
Sisi Mashia ni wafuasi wa
Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Mwanzilishi wa neno Shi’a kwa maana ya
“Wafuasi wa Ali” ni Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe. Kamwe hatumfuati mtu
binafsi bila rejea zenye hoja za kumuunga mkono.
Hafidh Abu Hatim Razi katika
kitabu chake “Az-Zainat” ambacho amekiandika kwa ajili ya kufafanua maana ya
maneno fulani na Semi zinazotumika miongoni mwa Wanachuo, anasema kwamba neno
la kwanza jipya ambalo lilikuja kukubaliwa na wote katika Uislamu wakati wa
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) lilikuwa ni “Shia.” Neno hili lilitumika kwa masahaba
maarufu wanne: Abu Dharr Ghifar, Salman Farsi, Mikdadi bin Aswad Kindi, na
Ammar Yasir. Hadith nyingi zaidi zilinukuliwa katika kuunga mkono nukta hii
hii.
Sasa ni juu yenu kufikiria vipi
iliwezekana kwamba wakati wa Mtume (s.a.w.w.) Wanne kati ya masahaba wake
wakubwa waliitwa Shi’a. Kama Mtume (s.a.w.w.) alifikiria kuwa neno hilo ni la
uzushi (bida’a), kwanini hakuwakataza watu kulitumia? Ukweli ni kwamba watu
walisikia kutoka kwa Mtume (s.a.w.w) mwenyewe kwamba wafuasi (Mashi’a) wa Ali
walikuwa ni wakazi wa Peponi. Walikuwa na fahari nalo na kwa uwazi wakajiita
wenyewe Mashi’a.
Kuanzia siku ya kwanza mpaka leo
Mashia wamekuwa wakiongoza kwa tabia nzuri za upole, usamehevu, kusaidia watu
wengine na kupenda amani na utulivu kwa wanadamu wote bila kujali dini zao wala
kabila.
Comments
Post a Comment