UIMAMU
NI NGUZO MUHIMU KATIKA UISLAMU
MWENYEZI
MUNGU ANASEMA: (Ewe mwanadamu! Ikumbuke) siku Tutakapowaita kila watu pamoja na
Imamu wao; basi atakayepewa kitabu (chake cha Amali) kwa mkono wa kulia, hao
watavisoma vitabu vyao (kwa furaha) (Bani Israeil, 17:71)
MTUKUFU
MTUME [s] AMESEMA: "Yeyote yule afaye pasi na kumjua Imamu wa zama zake,
atakuwa kafa kifo cha ujinga."
MTUKUFU MTUME [s] AMESEMA: "Hao (Ulul Amr watajwao mwenye Qur'ani 4:59) ni Makhalifa wangu na Maimamu wa Waislamu baada yangu. Wa kwanza ni Ali, kisha ni Hasan, kisha ni Husayn, kisha ni Ali bin Husayn, kisha ni Muhammad bin Ali, kisha ni Jaafar bin Muhammad, kisha ni Musa bin Jaafar, kisha ni Ali bin Musa, kisha ni Muhammad bin Ali, kisha ni Ali bin Muhammad, kisha ni Hasan bin Ali, kisha ni Muhammad bin Hasan (Mahdi)...." ("Kifayatul Athar" na "Rawdhatul Ahbab", vya Hafidh Jamaluddin Muhaddith).
Comments
Post a Comment