UISLAMU ULIANZA KWA
KUTANGAZWA UKHALIFA WA IMAM ALLY (A.S) KAMA KHALIFA WA KWANZA
Abu Muhammad Husain
al-Baghawi katika Tafsir Maalim at-Tanzeel
(inaojulikana kwa jina Tafsir al-Baghawi), Shaikh Alau’ddin Ali bin
Muhammad al-Baghdadi (anayejulikana kwa jina la Khazin al-Baghdadi) katika
kitabu chake Lubab al-tawil ambacho ni mashuhuri na kiitwacho Tafsir al-Kazin,
Abu Bakr Ahmad ibn Husayn al- Bayhaqi katika kitabu chake Dalail al-Nubuwwah,
Jalaluddin Suyuti katika kitabu chake Jami al-Jawami, Alau’ddin Ali al-Muttaqi
katika kitabu chake Kanzul Ummal, Abu Ja’far Muhammad ibn Jarir al- Tabari
katika Tarikh al-Rusul wal-Muluk (inaojulikana kwa jina Tarikh al-Tabari), Abi
Sa’adat Mubaraka Ibn Athir al-Jazari katika Tarikh al-Kamil, na Isma’il Abul
Fida katika Kitab al-Mukhtasar fi Akhbar- il-Bashar, wote hawa wamesema hivi:
kwamba Hazrat Ali amesema:-
“Iliposhuka aya “Waandhir Ashiratak-Al-Aqrabin” (Sura Ash-Shu’ara, aya 214)
Mtukufu Mtume akaniita na akaniamrisha, ‘Ee Ali Mwenyezi Mungu ameniamrisha
niwahadharishie watu wangu adhabu yake. Kwa kuona hali na tabia yao
nikiwafikishia maamrisho ya Mola watapinga kufanya yasiyofaa, basi
ikanihuzunisha sana na kudhoofika, kwa hivyo nikakaa kimya nikichelewesha zaidi
kutangaza maneno ya Mwenyezi Mungu basi ataishusha ghadhabu yake. Kwa hivyo Ee
Ali, chukua saa (kipimo) moja ya mchele, na tia mguu mzima wa mbuzi (kitoweo)
na bakuli kubwa la maziwa na utengeneze karamu; baadaye na uwaalike watoto wote wa Abdul Muttalib karamu kwangu
ili niwafikishie maneno ya Mwenyezi mungu.’
Basi nikafanya
alivyoniamrisha Mtume, na watoto wa Abdul Muttalib ambao walikuwa kiasi
arubaini ambao miongoni mwao walihudhuria Ammi zake Mtume: Abu Talib, Hamza,
Abbas na Abu Lahab. Hapo Mtume akaniamrisha nikalete hicho chakula, akachukuwa kipande cha nyama na akainyambua tena akazitawanya pembezoni mwa sinia na akasema,
“Kwa jina la Mwenyezi Mungu anzeni
kula”. Wote hawa waliohudhuria wakala
shibe yao ingawa chakula kile na bakuli la maziwa kilikuwa cha kumshibisha mtu mmoja tu.
Baadaye Mtume akataka kusema
nao lakini Abu Lahab mara akadaka maneno
na kusema, “Kweli rafiki yenu amekurogeni”. Kwa kusikia maneno haya wote
wakaondoka wakendazao, basi Mtume
hakupata fursa ya kusema nao.”
Siku ya pili Mtume akanitaka
nitengeneze chakula na kuwaita tena, basi nikafanya vivyo hivyo; wakaja wakala,
walipokwisha kula hapo Mtume akawahutubia hivi: “Enyi watoto wa Abdul Mutalib,
nimekuleteeni ninyi heri ya duniani na ahera, na Mwenyezi Mungu ameniamuru
nikwiteni mwende kwake (Mwabudu) yeye.
Kwa hivyo nani mwenye kuitikia
(kukubali) mwito wangu miongoni mwenu ili awe Waziri wangu, khalifa
baada yangu na ndugu yangu pia?”. Hapana mtu aliyeitikia. Lakini mimi (Ali)
ijapokuwa nalikuwa mdogo kuliko wote
katika kundi hilo nikasema, “Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi niko tayari hapa
kushika Wizara yako katika kazi hii”. Aliposikia Mtume maneno yangu,
akanipapasa shingoni kwa upole na akasema “Enyi watu wangu! Huyu Ali ni ndugu
yangu, waziri wangu na mwandani wangu
miongoni mwenu. Msikilizeni na mtiini huyu”.
Waliposikia maneno ya Mtume, mara wakacheka kwa sauti na wakaondoka huku wakimwambia Abu Talib,
“Sikiliza! Umeamrishwa kumtii na kumfuata mtoto wako”.
Toleo hili vile vile
limetanjwa na Thomas Carlyle katika kitabu chake Heroes and Hero Worship, vile vile Edward
Gibbon katika kitabu chake Decline and Fall of the Roman Empire, John Davenport
katika Apology for Muhammad and the Koran, na mwishoni Washington Irvin
katika Muhammad and His Successors, na
maelezo yake yote.
Hivyo ukhalifa wa Imam Ally
ulitangazwa na Mtume kuanzia siku ya kwanza ya kuutangaza Uislamu. Nasi kama
tunataka kheri katika dunia hii na akhera hatuna budi kujiunga na ukhalifa huu
wa imam Ally (a.s) na Ahlulbayt wake. Na ili tuwe wafuasi wa ukhalifa wa imam
Ally ni lazima tuwe Mashia Imamiya.
Comments
Post a Comment