FADAK
Fadak ni shamba
lilokuwa kaskazini ya Madina, umbali wa safari ya siku 2 au 3, ilikuwa ni ardhi
yenye rutuba sana, kwa mujibu wa Ibn Abi Hadid, vijisitu vya tende havikuwa
vidogo kama vile vya Kufa ambazo pato lake lilikuwa kati ya 24,000 dinar.
Ilikuwa inakaliwa na kabila la Mayahudi.
Katika mwaka wa 7 A.H.,
Mtume alipigana vita dhidi ya Mayahudi wa Khaibar, kwa sababu walivunja mkataba
na Waislamu. Baadhi ya ngome zao zilichukuliwa; mbili au tatu zilizingirwa.
Mwishowe walipendekeza mpango ambao
maisha yao, dini, heshima yao nk. itakuwa salama, na wataondoka katika ngome na
kufanya kazi za shamba kwa ajili ya
Waislamu. Mapatano yalifikiwa; Mayahudi
waliruhusiwa kufanya kazi kwenye mashamba kwa niaba ya Waislamu na mazao
yaligawanywa kati ya Mayahudi na Waisalmu nusu kwa nusu.
Kwa mujibu wa aya ya
Qur’an (8:41) moja ya tano ya ngome na ardhi alipewa Mtume kama Khums, na nne
ya tano iliyobakia ilikwenda kwa Waislamu.
Wakati Mayahudi wa
Fadak waliposikia vita ya Khaibar na matokeo ya makubaliano, walianza kufikiria
kuhusu wao wenyewe. Wakati huo huo akaja mjumbe kutoka Madina, akawalingania
Uislamu. Walikataa kukubali Uislamu,
lakini kwa matakwa yao wenyewe,
walikubali amani kwa masharti yafuatayo:
a. Watatoa nusu ya
ardhi yao kwa Mtume, nusu iliyobaki iwe
kwenye miliki yao.
b. Watafanya kazi
katika ardhi ya Mtume na kugawana mazao yake.
c. Mtume atakuwa na
mamlaka ya kuwafukuza kutoka Fadak wakati wowote atakao, lakini itampasa
kuwalipa malipo kamili ya mgao wao wa ardhi na mali yao.
Mtume alikubali
masharti yao3.
Baadhi ya Waislamu
walifikiri kwamba Fadak ilikuwa vile vile mali ya Waislamu kama Khaibar. Lakini ni kutokuelewa kwao, kwa sababu zamani
kabla ya hilo, katika suala la Banu
Nazir, sheria ilitangazwa rasmi kwamba chochote
kinachokuja kwa Mtume bila ya kupigana vita, kitakuwa ni mali binafsi ya Mtume, kwa ajili ya matumizi yake
au kugawa kwa atakaeona inafaa, na
Qur’an inasema:
“Na mali aliyoleta
Allah kwa Mtume Wake hamkuyakimbilia mbio kwa farasi wala ngamia. Lakini Allah
huwapa mamlaka Mitume Wake juu ya wowote awatakao, na Allah ana uwezo juu ya
kila kitu.” (59:6)
Banu Nazir walifukuzwa
kutoka Madina mwanzoni mwa mwaka wa tatu
hijiriyya. Waliruhusiwa kuchukuwa chochote kile
kinachowezwa kubebwa na ngamia wao isipokuwa silaha.
Katika kuwasili kwake
Madina, Mtume alifanya uhusiano wa
kindugu, akimfanya Muhajir ndugu wa Ansar na kila Ansar aligawa mali
yake yote nusu kwa nusu na ndugu yake Muhajir, kiasi kwamba kama mirathi ya Ansar ilikuwa ikigawanya
miongoni mwa kaka na dada zake, ndugu
Muhajir alijumuishwa ndani yake.
Abu Bakar alifanywa
ndugu na Kharijah bin Zayd; ‘Umar na ‘Utban bin Malik Ansari walifanywa ndugu,
kama walivyofanywa ‘Uthman na Aws bin Thabit Ansar, na kadhalika Ali peke yake
aliachwa nje ya undugu huu, Mtume alitangaza kwamba Ali ni ndugu wa Mtume
mwenyewe.
Alipopata mali ya Banu
Nazir, Mtume kwa matakwa yake mwenyewe
aliamua kuigawa miongoni mwa Muhajirin na akawaondolea Ansar mzigo huu. Alifanya hivyo, na
akawajumuisha katika orodha hii Ansar wawili masikini sana - Abu Dajjanah na
Sahl ibn Haneef.
Hivyo Muhajirin wote,
wakiwemo Abu Bakar, ‘Umar na ‘Uthmani walipata mgao wao kutoka kwenye ardhi hiyo
na ikawa mali yao binafsi. Haikuwa kwa
ajili ya “kujikimu” tu.
Katika njia hiyo hiyo
Fadak ikawa mali ya binafsi ya Mtume na
aliisimamia yeye mwenyewe.7
Kisha aya nyingine ya
Qur’an ilikuja: “Na mpe jamaa yako wa karibu haki yake....” (17:26)
Mtume alimuuliza Jibril
maana ya aya hii. Akasema: “Mpe Fatimah
Fadak; itakuwa ni chanzo chake cha mapato na watoto wake.”8
Mtume akampa Fatimah Fadak; na alikuwa akiitumia kama mali yake mwenyewe;
wakala wake alikuwa kule akiangalia maslahi yake. Hii iliendelea mpaka Mtume
alopofariki na Abu Bakar akachukuwa
umiliki wa Fadaka kwa nguvu.
Fatimah alipinga dhidi
ya uporaji huu wa mali yake, akisema
kwamba Mtume alimpa yeye. Abu Bakar akamuambia
alete mashahidi kuthibitisha jambo hili.
Sasa Fatimah alikuwa
tayari katika umilki wa mali hii; na kwa
mujibu wa kanuni za ki-Islamu, umiliki wenyewe ni uthibitisho wa kutosha
wa umilikaji. Kama Abu Bakar alidai mali ile kwa ajili yake mwenyewe au kwa
ajili ya taifa la ki-Islamu, basi ni yeye, kama mdai ambaye alipaswa kuleta
mashahidi kuunga mkono madai yake. Lakini aliweka dhima ya kuthibitisha juu ya
Fatimah, akipuuza Sheria ya ki-Islamu.
Huu ni uthibitisho wa
dhuluma walizofanyiwa Ahlulbayt wa Mtume kutokana ubabe wa watawala waliojiita
wenyewe kuwa ni makhalifa wa Mtume. Ukweli ni kuwa Mtume hawezi kumpa ukhalifa
mtu anayedhulumu mali za watu tena alianzia dhulma kwa kuwadhulumu wanafamilia
wa Mtume.
Rejea
3. Yaqut Al-Hamawi,
Mu’jamul-Buldan; Ibn Abil Hadid, Sharh Nahjul Balaghah j.16 uk.210; al-Tabari, Annals, J. Uk. ;
Ibnul Athir, Tarikhul Kamil.
6 Tafsir
Ad-Durr’l-Manthur, j.6 uk.187-190 7 Ar-Razi, Tafsir Kabir, Az-Zamakhshari,
Tafsir Al-Kashshaf
8 Suyuti,
Ad-Durrul-Manthur, j.4, uk.177; Suyuti, Lubabun-Naqul, imechapishwa katika pambizo laTafsir al-Jalalain, j.2,
uk.19.
Comments
Post a Comment