FAMILIA KATIKA UISLAMU

FAMILIA KATIKA UISLAMU
Familia katika Uislamu, ina utaratibu mzuri na wa hali ya juu sana, na ni utaratibu unaoheshimiwa sana na ni mahali panapostahiwa. Ni kwa sababu hii na ndio maana Uislamu huipa nguvu (familia).

Ndoa ndio mwanzo wa kuunda familia na kisha jamii, na uangalifu wa Uislamu katika nguzo hiyo muhimu, hatimaye unaongoza kuelekea katika maisha ya amani na furaha.

Qur’an (60:11)   imendikwa: Enyi mlioamini, watakapo- wafikieni wanawake waaminio wanaohama, basi wajaribuni, Mwenyezi Mungu ndiye Ajuaye zaidi imani yao, kama mkijua kuwa wao ni waaminio basi msiwarudishe  kwa makafiri. (Wanawake) hawa si halali kwao, wala wao (wanaume makafiri) si halali kwao; na warudishieni waume zao mali walizotoa. Wala kwenu si hatia kuwaoa  ikiwa mtawapa mahari yao; wala msiwaoe wanawake makafiri, na ombeni mliyoyatoa, nao waombe walivyovitoa. Basi hii ndiyo hukumu ya Mwenyezi Mungu Anayowa- hukumu kati yenu; na Mwenyezi Mungu ndiye Ajuaye, Mwenye hekima.

Hii ni miongoni mwa aya nyingi zinazofafanua kuwa waislamu tunatakiwa kuwaoa wanawake wema na waislamu. Kuna athari kubwa endapo kama mtu ataoa au ataolewa na mtu asiyekuwa mwislamu au mtu anayedai kuwa ni mwislamu lakini hafuati maadili ya kiislamu. Maisha yao ya kiroho yatakumbwa na vikwazo vingi na malezi ya watoto yatakuwa magumu kabisa maana kila mmoja atakuwa anajitahidi kuvutia watoto upande wake, hatimaye watoto wataharibika.


Taasisi hii muhimu ya familia inatakiwa iundwe kwa umakini na pia isimamiwe kwa umakini kwa kuwalea watoto vizuri kwa kuwasomesha elimu zote, lakini elimu ya awali ihusiane na kumpenda Mwenyezi Mungu, Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Ahlulbayt wake. Mtoto aliyelelewa kwa misingi hii tunaamini kuwa atakuwa mwema. 

Comments