JE IBILISI NI MALAIKA AU JINI AU NANI HASA?

JE IBILISI NI MALAIKA AU JINI AU NANI HASA?
Qur'an imeandikwa; Na Tulipowaambia Malaika: Msujudieni Adamu! Wakasujudu ila Iblis, akakataa na alikuwa miongoni mwa makafiri (2:34).
Ibilis hakuwa Malaika; maana Mwenyezi Mungu anasema, Malaika 'hawamwasi Mwenyezi Mungu Aliyowaamuru, na hutenda wanayoamrishwa" (66:7); lakini Ibilisi aliasi, hivyo hakuwa Malaika.

Katika Aya hii Mwenyezi Mungu amefupisha maneno na inaonekana Ibilisi kana kwamba alikuwa mmoja wa Malaika. Lakini katika sura 7:13 Mwenyezi Mungu anaonyesha kuwa Ibilisi pia alipewa amri ya kumtumikia Adamu lakini hakutii, ndipo Mwenyezi Mungu akamkasirikia.
Sura 18:51 inaeleza kuwa Ibilisi alikuwa miongoni mwa jinn (viumbe wa siri) ambao, kinyume na Malaika, wao walipewa uwezo wa kutii na kuasi.
Iblisi ni jini lililokuwa linaishi na malaika kwa muda mrefu na ilipotolewa amri ya kumtii adamu yeye pekee ndiye aliyegoma na hivyo kulaaniwa na Allah na kufukuzwa toka katika neema za Allah. Iblisi alimwomba Mwenyezi Mungu ampe muda mrefu ili aweze kumpotosha Adam na watoto wake. Mwenyezi Mungu akampa ruhusa hiyo. Kuanzia siku ile mpaka leo anaendelea na kazi yake ya kuhakikisha kuwa watu hatumtumikii Allah ipasavyo na hivyo twende Jahannam pamoja naye.
Allah ameahidi kuwa hatoruhusu Ibilis awapotoshe watu wacha Mungu, lakini wale wataoafikiana na shetani (ibilis) wakusanywa pamoja na kujazwa ndani ya Moto wa Jahannam siku ile ya hukumu.

Tunamwomba Allah atulinde kutokana na upotoshaji wa Shetani (ibilisi) na majeshi yake. 

Comments