KHALIFA AU IMAMU WA TATU WA WAISLAMU

KHALIFA AU IMAMU WA TATU WA WAISLAMU

Naye ni Hussein bin Ali bin Abi Talib (a.s.), na mama yake ni Bibi Fatima, binti yake Mtume (s.aw.w.), na yeye ni mjukuu wa Mtume (s.a.w.w), ni wa tatu katika Makhalifa, na ni baba wa maimamu tisa baada yake, na ni Imam wa watu baada ya kaka yake (Imam Hassan)   (a.s.).
Kazaliwa katika Madina Munawwara, mwezi tatu Shaaban, mwaka wa nne wa Hijiria.
Kauwawa hali ya kudhulumiwa kwa upanga katika hali ya kiu, katika mapigano ya Ashura [6] yaliyoko mashuhuri, siku ya Ijumaa, mwezi kumi mfungo nne mwaka wa sitini na moja wa Hijiria, na akasimamia mambo ya mazishi yake baada ya siku tatu mtoto wake Ali Zainul Abediin (a.s.), akamzika mahala lilipo kaburi lake sasa katika mji wa Karbala Mtakatifu.
Fadhila zake hazitajiki. Yeye ni manukato ya Mtume (s.a.w.w.), kama alivyo sema Mtume (s.a.w.w) kwa yeye na kwa kaka yake Imam Hassan (a.s): "Wao ni manukato yangu duniani".
Na akasema Mtume (s.aw.w.): "Hussein ni katika mimi na mimi ni katika Hussein." Pia akasema: "Hassan na Hussein ni maimamu ijapokuwa wamesimama au wamekaa."
Alikuwa mwenye elimu kubwa na mwabudu mno, alikuwa anasali kila usiku elfu rakaa kama baba yake Amirul muuminiin Ali (a.s).
Alikuwa anabeba siku nyingi mifuko ya vyakula kuwapelekea mafakiri, mpaka ikaonekana alama ya mizigo baada ya kuuwawa kwake; na alikuwa mkarimu, mpole na alikuwa anaghadhibika anapoona mtu akifanya kinyume cha sheria ya kiislamu.
Na katika ukarimu wake, ni kuwa Mwarabu mmoja alimkusudia kwa kutaka haja yake. Akamfanyia mashairi (nashidi), akasema:-
"Hakurudi utupu ambaye akakutumai na akakusudia mlangoni kwako."
"Wewe ni mkarimu na wewe mwenye kutegemewa: baba yako alikuwa muuwaji wa fasiki (wale wanaomwasi Mwenyezi Mungu)."
"Lau si ambayo yamekuwa kutoka kwa wazee wenu, ungalitufunika moto wa Jahannam."
Imam Hussein (a.s.) aliposikia nashid hii akampa dinari elfu nne, na pia akamtaka msamaha kwa mashairi haya:-
"Chukua hizi, mimi kwako ninataka msamaha, jua kuwa mimi ni mwenye huruma kwako.
"Lau tungalikuwa na fimbo katika mwenendo wetu wa mapema yangalikuwa mawingu yetu juu yako yenye kunywesha (kama ungalikuwa utawala wa dola ya Islamu mkononi mwetu, tungalikusaidia zaidi).
"Lakini khadaa ya zama ina migeuzo, na kitanga changu ni kichache cha nafaka (matumizi)."
Akaishia (a.s.) kwa msimamo wake wa ushujaa (ambao hapana mfano ulimwenguni) sharia za Ki-Islamu na dini ya baba yake Rasulullah (s.a.w.w), kamwe kuhuisha ulimwengu mzima mpaka siku ya kiyama.

Yeye ni bwana wa mashahidi na mbora mno baada ya kakaye.

Comments