MAJIBU KWA WANAOPINGA
KUOA WAKE WENGI
Upinzani wa wasiokuwa
waislamu juu ya jambo hili kwa hakika unachusha. Wanapenda kulaumu bila kujali ubora wa jambo
lenyewe ila tu kwa kuwa wao wenyewe hawanalo
jambo hili kwa ajili ya kuharibiwa na watangulizi wao.
Padre Dale
anasema. Wakristo hawawezi kuiamini
Qur'an kwa kuwa Vitabu vyao havipatani na
Qur'an (uk. 583). Sisi tunauliza, Je, Ukristo unapatana na mafundisho ya Agano
la Kale? Mbona wanaamini Agano la Kale pia?
Katika shauri la vyakula, ibada na hukumu nyingine za dini, Ukristo ni
mbali na Agano la Kale, lakini juu ya kuhitilafiana hivyo, wanaamini Agano la
Kale pia.
Kadhalika Padre Dale
anasema. "Mkristo hapewi ruhusa katika Injili kuwa na wake wawili, sembuse
wanne" (uk 569). Lakini Injili
inasema, Yesu alisema, "Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua Torati au manabii;
la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.
Kwa maana, amin, nawaambia, mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi
moja wala nukta moja ya Torati haitaondoka, hata yote yatimie. Basi mtu ye yote
atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo,
ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na
kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni (Matt.
5:17-20).
Tena Yesu akasema
"Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa; basi yo yote watakayowaambia myashike na
kuyatenda" (Matt. 23:2).
Je Torati iliharimisha
kuoa wake zaidi? Torati inasema, Akiwa
mtu ana wake wawili, mmoja ampenda, mmoja hampendi, nao wamemzalia vijana . . .
na yule mzaliwa wa kwanza akiwa ni wa mke asiyependwa; ndipo itakapokuwa ya
kwamba siku atakayowarithisha wanawe alivyo navyo, na asimweke mwana wa
ampendaye kuwa mzaliwa wa kwanza mbele ya mwana wa asiyempenda,"
(Kumbukumbu 21:15-17).
Pia soma Kumbukumbu la
Torati (25:5). Je, maneno hayo hayaonyeshi kuwa kuoa zaidi
hakulaumiwi? Ni wazi Wakristo wanapinga
maneno ya Yesu aliyewaambia wafuate amri zote
za Torati na maneno ya Manabii na
ya Mashekhe wa Kiyahudi.
Comments
Post a Comment