MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {V}

MATENDO MATUKUFU KWA MUISLAMU {V}

{1}Kusameheana:
Mwenyezi Mungu amesema: "Na mkiwasamehe na kupuuza yaliyopita na kuyafuta kabisa katika nyoyo zenu {basi Mwenyezi Mungu} atafurahi kwani Mwenyezi Mungu ni Msamehevu, Mwingi wa rehema." {Qur'an, Sura ya 64, aya ya 14}.

{2}Kukidhi haja za watu:
Mtukufu Mtume {s.a.w.w.} amesema: "Mwenye kukidhi haja ya nduguye mwenye kuamini {Muislamu} basi kama amefanya ibada ya Mwenyezi Mungu maisha yake."

{3}Kufanya usawa kwa kila kitu:           
Mtukufu Mtume {s.a.w.w.} amesema: "Unachopendelea kwa ajili ya nafsi yako, wapendelee wenzio pia. Fanya usawa kati ya wake zako kama unao wengi na kati ya wanao, wala usipendelee kabisa."


Mwenyezi Mungu amesema: Lawama iko juu ya wale wanao dhulumu watu na wakawafanyia jeuri katika ardhi pasipo haki. hao ndio watakao pata adhabu. {Qur'an, Sura ya 42 aya ya 42}

Comments