MAWAHHABI SIO MASUNNI BALI HUWAHADAA MASUNNI ILI KUWAPOTOSHA

MAWAHHABI SIO MASUNNI BALI HUWAHADAA MASUNNI ILI KUWAPOTOSHA
Wako watu wanaoamini kuwa Ibn Taimiya ni kiongozi wao; na hivyo ndivyo waaminivyo Nasibi, Salafi swaleh, wahhabi, Answari Sunna na Kharji. Watu hawa ili kuwahadaa Masunni, hujitokeza kama Masunni lakini ukweli ni kuwa hawa sio Masunni kwa sababu huenda kinyume na mengi ya mambo wanayoamini Masunni.
Kwa mfano Masunni kama mashia huamini kuwa Mwenyezi Mungu hana viungo kama vile miguu, mikono, macho n.k lakini Mawahhabi huamini kuwa Mwenyezi Mungu anayo miguu na mikono tena hukaa kwenye kiti cha enzi. Imani yao hii ni ukafiri wa wazi na wanachukua jitihada zote ili kuwapotosha Masunni na kuwangiza katika ukafiri huu.

Watu hawa vile vile humchukulia Yazid (yaani Muuaji wa Imam Hussein (a.s)) kuwa ni khalifa wa kweli na hivyo, Mwenyezi Mungu na atusamehe, humchukulia Imamu Husayn (a.s) kuwa yu mwenye makosa aliyestahili kuuawa.

Siku hizi, maoni ya namna hii yanatolewa na Mahmud Ahmad Abbasi, ambaye kitabu chake kiitwacho "Khilafat Muawiya wa Yazid" kimeziumiza hisia za Waislamu wengi. Kwenye siku za awali, kabla ya Ibn Taimiya (aliyefariki mnamo mwaka 728 Hijiriya), mtu mmoja aliyeitwa Abu Bakr Muhammad bin Abdullah bin al-Arabi (aliyefariki mnamo mwaka 543 Hijiriya) alijitokeza kwenye itikadi hiyo hiyo. Mtu huyo aliandika hivi: "Husayn hakuuawa ila kwa upanga wa babu yake mwenyewe (yaani kwa mujibu wa kanuni za shari'ah), kwa sababu kililiwa kiapo cha utii kwa Yazid na hivyo Husayn alikuwa mwasi".

Angalia maneno ya Imamu Ghazali {huyu ndie yule yule aliye maarufu kwa jina la Hujjatul Islam na anaaminiwa kuwa yu nguzo ya kanuni za kidini (za Kisunni)} alitoa fatwa kuwa: "Ni haramu kuhadithia juu ya Husayn na wafuasi wake kwenye hotuba, kwa sababu kufanya hivyo kunazaa chuki juu ya masahaba". Ni dhahiri kwamba, kama Imamu Ghazali aliifikiria sehemu ya Imamu Husayn (a.s) kuwa ni ya haki, asingeharimisha kuihadithia. Tukiyafikiria yote haya, mtu hatakuwa na jingine la kufanya ila kuamua kuwa, Ulama kama hawa hawamfikirii Imamu Husayn (a.s) kuwa yu mtu mtukufu na kwamba, kwa mujibu wa maoni yao, kukataa kwa Imamu Husayn (a.s) kula kiapo cha utii kwa Yazid kulikuwa ni kosa kubwa mno kiasi kwamba hadi hivi leo wanaandika kuwa, Mwenyezi Mungu na atusamehe Imamu (a.s) alikuwa na dalili za ukaidi.


Hii ni dhahili kuwa Mawahhabi, masalafi, Answari Sunnah na wengineo wenye misimamo kama yao ndio wauaji wa Imam Hussein na ndio sababu ya wao kufurahia mauaji hayo. Allah awalaani wauaji wa imamu wetu huyu.

Comments