NINI ITIKADI YA MASHIA
JUU YA UIMAMU?
Jibu: Mashia wanaamini
kwamba Mtume Mtukufu (s.a.w.) aliwachagua Makhalifa (Maimamu) Thenashara (12) kwa amri ya Mwenyezi Mungu na
akawataja kwa majina yao. Wao
wamehifadhika kutokana na kila dhambi na
kosa kama Mtume Mtukufu (s.a.w.) alivyo,
ambaye kwa ajili ya sifa zake Mwenyezi Mungu amesema: “Hasemi kwa
matamanio yake, ila tu ni Wahyi (ufunuo) aliofunuliwa.” (Qur’an, 53:3).
Hao makhalifa 12 ni:
1. imam Ali Amirul Mu’miniyn,
2. imam Hassan,
3. imam Husayn,
4. imam Ali bin Husayn,
5. imam Muhammad Baqir,
6. imam Ja’far Sadiq,
7. imam Musa Kadhim,
8. imam Ali Ridha,
9. imam Muhammad Taqi,
10. imam Ali Naqi,
11. imam Hassan
Askariy, na
12. imam Muhammad Mahdi
(Amani iwe juu yao wote).
Majina yao na Ukhalifa
wao vimeandikwa kufuatana na hadithi za
Mtume katika vitabu vya Kisunni na vya Kishia pia.
Comments
Post a Comment