UIMARA WA WATU WENYE IMANI THABITI

UIMARA WA WATU WENYE IMANI THABITI
Tutatumia hadithi inayomhusu Firauni na wachawi wake, tunasoma kwamba aliwaita waganga wake wote wa mazingaombwe ili wamshinde Musa (a.s) yule mtu aliyesemeshwa na Mwenyezi Mungu, wakiwa na matumaini kwamba kwa werevu na uwezo wao wa kichawi, wangeweza kumlazimisha kusalimu amri kwa firaun aliyekuwa akidai kuwa yeye ni Mungu na kwamba aabudiwe.
Lakini shukrani kwa uwezo wa kimiujiza aliopewa Musa, walishindwa na wakarejea kwenye imani ya kweli. Firauni mwenye hasira, ambaye kiburi chake kilivunjwa, akaanza kuwakashifu na kuwatishia, akiwaambia kwamba angewaadhibu kwa mateso mabaya kuzidi yote - yaani kuwakata miguu yao. Lakini, mageuzi ya kina sana yalikwisha kufanyika katika nyoyo zao; walibakia kuwa imara na madhubuti mbele ya vitisho na kurairai kwa Firauni na mateso yake makali. Wachawi hao wakajibu, kwa ushupavu sana; "....basi fanya unavyotaka kufanya, unaweza kutoa hukumu inayohusiana na maisha haya ya dunia tu." (Surat-Twaha; 20:72).

Comments