VITA VYA JAMAL AU VITA
VYA BASRA
Hii ni vita ya pili ya
waislamu kwa waislamu yaani wenyewe kwa wenyewe. Vita ya kwanza iliendeshwa na
Abubakar bin Quhafa pale alipotuma jeshi chini ya uamiri wa Khalid bin Walid
kwenda kuwateketeza waislamu waliogoma kutoa zaka ikiwa ni mbinu ya kuugomea uongozi
wake batili. Matajili hawa walifahamu wazi kuwa khalifa wa kwanza aliyetangazwa
na Mtume Muhammad (s.a.w.w) ni imam Ally bin Abi Talib (a.s). Khalid bin Walid
waliwafyeka wote waliogoma kutoa zaka.
Mama yetu Aisha (R.A)
alikuwa akirejea Madina akitoka Hijjah aliposikia taarifa ya kuuawa Uthuman bin
Affan na pia taarifa za ukhalifa wa Imam Ally. Kwanza aliamua kurudi Makkah na
kufanya mkutano na watu kadhaa ili kuunda jeshi la kumpiga vita imam Ally (a.s).
alifanya mkutano na kundi kubwa la maadui wa imam Ally akiwemo Zubeir, Twalha
na bani Umayya ambao wamekuwa na uadui wa jadi dhidi ya ukoo wa Mtume yaani
Bani Hashim. Ukoo huu ndio ulioongoza mateso na mauaji dhidi ya Ahlulbayt wa
Mtume na mti uliolaaniwa katika Qur’an.
Kikao hiki kiliamua
kupeleka jeshi kupambana na imam Ally na wafuasi wake kwa madai ya kuwa
wanalipiza kisasi dhidi ya mauaji ya Uthuman bin Affan. Walikusanya askari
30,000 na kuelekea Basra na kuuteka mji huo ili kuufanya kuwa ngome yao katika
kumshambulia Imam Ally (a.s) na jeshi lake. Walifanikiwa kuuteka mji huu lakini
hawakufanikiwa kuwashawishi wenyeji wa mji huu kushirikiana nao katika vita
vyao dhidi ya Khalifa Imam Ally (a.s), hivyo wakawaua waislamu 600. Hii ni
pamoja na kumteka gavana wa mji huu Uthuman bin Hunaif akiwa msikitini na
kuwaua waumini 40 waliokuwa waswali.
Hii ilikuwa ni mbinu ya
kuficha ukweli kwani waliamini kuwa imam Ally ni Mtu wa haki na angefanya
uchunguzi dhidi ya mauaji yale kwa hiyo wakaona kuwa ili kuwaficha wauaji ambao
walikuwa miongoni mwao ni lazima waanzishe vita dhidi ya imam Ally na
kumshughulisha vita ili asahabu kumtafuta muuaji halisi wa Uthuman.
Bani Umayya ni kabila
la Uthuman, walishirikishwa katika vita hii kwa sababu kwanza aliyeuawa ni
ndugu yao lakini wao wanajulikana kwa uadui wao dhidi ya Mtume na Ahlulbayt
wake na hivyo walifahamu fika kuwa Bani Umayyah hawatosita kushiriki vita dhidi
ya Imam Ally (a.s).
Ukweli ni kuwa kama
ukhalifa usingechukuliwa na imam Ally, vita hiyo isingetokea. Walimpiga vita
imam Ally na serikali yake kwa sababu ya chuki zao dhidi ya Ahlulbayt. Na lengo
hasa la bi Aisha ni kuweka khalifa mpya, Abdullah bin Zubeir, mwipwa wake na
mwanae wa kupangwa.
Magavana mafisadi
waliotolewa madarakani na imam Ally (a.s) yaani Abdullah bin Amir wa Makkah, Ya’la
bin Umayya wa Yemen na Abdullah bin Kuraiz wa Basra, waliungana na jeshi hilo
la wanafiki.
Mughira bin Shuba
aliwashauri kuwa kule wanakokwenda hakuna wauaji wa Uthuman, wauaji halisi na
majenerali wao waliopo katika jeshi hilo na lengo lao ni kupata ukhalifa basi. Jeshi
hili haramu lilipinga na kusonga mbele.
Baadaye alifika eneo
liitwalo Hauab, mbwa wakamzunguka bi Aisha na kumbwekea sana. Aisha alihamanika
sana akauliza ni eneo gani hilo? Wenyeji wa hapo wakamjibu kuwa eneo hilo ni
Hauab. Hapo ndipo alipohamanika zaidi na kukumbuka hadith ya Mtume iliyomlaani
mke wake atakayebwekewa na mbwa wa Hauab. Akaagiza arudishwe Makkah lakini watu
wake wakatafuta mashahidi 50 wa uongo ili wamdanganye kuwa eneo hilo si Hauab. Wakafanikiwa
kwa hilo hivyo wakaendelea na safari zao za Shari.
Imam Ally aliposikia
habari hii aliandaa jeshi la askari 6000 na kuelekea Basra ili kukabiliana na
jeshi hilo la waasi. Kwanza aliwatumia barua ya kuwasihi waache uasi. Watu hawa
walipinga na kusonga mbele.
Ndipo imam Ally (a.s)
alipoamua kukabiliana na waasi hao na kuwashinda kwa muda mfupi sana. Vita hii
iligharimu maisha ya waislamu zaidi ya elfu kumi akiwemo Twalha.
Vita ilimalizika kwa
kukamatwa bi Aisha na mateka wengine kutoka upande wa wanafiki. Imam Ally
akawasamehe na bi Aisha kukabishiwa kwa kaka yake Muhammad bin Abubakar
aliyekuwa Mshia maarufu na alipigana vita ile akiwa upande wa imam Ally na sio
dada yake.
Tunajifunza hapa kuwa
tuwe makini tunapofanya maamuzi kwani taarifa nyingi tuzipatazo zinaweza
kupelekea vita na umwagikaji wa damu za watu wasiokuwa na hatia kama walivyo
fanya Aisha na jeshi lake.
Comments
Post a Comment