AJABU YA MWIZI KUWA
HAKIMU
(DHULMA ZA ABUBAKAR
DHIDI YA AHLULBAYT)
Baada tu ya Mtume
kufariki dunia, Abubakar bin Quhafa (r.a) alinyakuwa ukhalifa kwa msaada wa
Umar bin Khatab (r.a). alipokalia kiti cha kwanza ilikuwa kuwalazimisha watu
wamtii na wale waliopinga waliuawa mara moja.
Kisha alipora mali za
Mtume na kuzichukua kwa madai kuwa Mitume hawarithiwi. Madai haya ya Abubakar
yalikwenda kinyume na maelekezo ya Qur’an takatifu ambayo inasema kuwa watu
wote warithiwa. Kwa kuwa Mtume alikuwa mtu bila shaka anarithiwa. Na wale
wanaoendeleza madai haya ya uongo kwamba mitume hawarithiwi watueleze au
wathibitishe kuwa Mtume Muhammad hakuwa mwanadamu.
Kumbuka kipindi hicho
Abubakar ndio sasa kiongozi wa waislamu na ukitaka haki ni lazima umfute yeye. Bint
wa Mtume (s.a.w.w), yaani Fatuma alikwenda mara kadhaa kwa Abubakar kudai sio
tu mirathi yake bali shamba lake aliloporwa na kiongozi huyo. Majibu yakawa ni
yale yale, mitume hawarithiwi.
Tena, kwa vile Abubakar
alikuwa ni mshitakiwa, hakupaswa kuhukumu kesi yeye mwenyewe. Lakini hakujali mambo ya undani ya
kimahakama ilimradi tu madhumuni yake
yametekelezwa.
Hata hivyo, Fatimah
alimleta Ali na Umm Ayman (mjane wa Zaid bin Haritha) kama mashahidi wake ili
kuthibitisha kuwa shamba (FADAK) alilonyang’anywa ni mali yake ya halali
aliyopewa na Mtume (s.a.w.w) miaka miwili kabla ya kifo chake. Abu Bakar akaupinga ushahidi wa imam Ally na Umm
Ayman, akasema lazima kuwe na amma wanaume wawili au mwanaume mmoja na wanawake wawili kama
mashahidi.
Ukweli ni kuwa, katika
masuala ya familia - zawadi ya baba kwa bint yake ni suala la familia - shahadi
mmoja tu anatosha; lakini Abu Bakar kwa urahisi alilisahau hili. Vile vile Uislamu
hukubali shahidi mmoja aliye ungaunisha
na kiapo cha mdai kama uthibitisho wa kutosha.
Fatimah alilazimika
kuleta mashahidi wengine, miongoni mwao ni watoto wake wawili, Hasani na
Huseini na mwanamke mmoja, Asma bint Umais (mke wa Abu Bakar mwenyewe).
Sasa kulikuwa na
mashahidi zaidi kuliko kiwango cha chini
kilichotakiwa. Hivyo Abu Bakar alianza kushusha sifa za mashahidi wote:
Rejea
Fakhuruddin Ar-Razi,
Tafsir Kabir, j.8, uk.386.
Kanzu ’l-‘Ummal, j.3
uk.178-9
Comments
Post a Comment