IMAM SHAFII (R.A) ALIKUWA MSHIA
Allah (s.w) anasema, "Shikamaneni
na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msitengane". (3:103). Tamko la kamba
hapa ni AHLUL BAIT". na hapa tutaonyesha maneno ya Imam Shaafy "Na
nilipowaona watu Madhehebu yao yamewapeleka katika bahari ya ya upotovu na
ujinga, nikapanda kwa jina Ia Mwenyezi Mungu katika meli yenye kuokoa, nao ni
watu wa nyumba ya Mtume, mwisho wa Mitume. Na nikaishika kamba ya Mwenyezi
Mungu nayo ni kuwatawalisha (Ahlul Bait) kama tulivyoamuriwa kushikamana na
kamba, watakapo farakana katika dini makundi sabini na kidogo kama ilivyokuja
katika Hadithi.
Na asipatikane wa kuokoka miongoni mwao isipokuwa kundi moja, niambieni ni
kundi gani hilo enyi wenye akili na maarifa, je! Katika makundi yatakayoangamia
mojawaponi ni lile kundi la watu wa Muhammad? Au wao ni katika kundi litakalo
salimika, niambieni. Ikiwa utasema kundi la Muhammad ni katika kundi
litakalookoka, basi huo ni msimamo wa kweli, na ukisema kundi hilo ni katika
makundi yatayoangamia bila shaka umepotosha uadilifu, basi niachie Ali awe
kiongozi wangu na kizazi chake, na wewe bakia katika mapambo ya ulimwengu."
Imam Shaafy hapa anatukumbusha tamko muhimu Ia Mtukufu Mtume (s.a.w.) aliposema: "Mfano wa Ahlul Bait wangu ni kama mfano wa Meli ya Nuhu, atakaepanda humo ataokoka, na atakaebaki nje atazama".
Tazmaa: Manaqib Ali Uk. 132
Mustadrakus Sahihain J.2 Uk. 343
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 168
Kanzul Ummal J.6 Uk. 216
Hilyatul Awliyaa J.4 Uk. 306
Imam Shaafy hapa anatukumbusha tamko muhimu Ia Mtukufu Mtume (s.a.w.) aliposema: "Mfano wa Ahlul Bait wangu ni kama mfano wa Meli ya Nuhu, atakaepanda humo ataokoka, na atakaebaki nje atazama".
Tazmaa: Manaqib Ali Uk. 132
Mustadrakus Sahihain J.2 Uk. 343
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 168
Kanzul Ummal J.6 Uk. 216
Hilyatul Awliyaa J.4 Uk. 306
Imepokewa kutoka kwa Sahaba Zaid bin Arqam: Amesema Mtume (s.a.w.):-
"Mimi ninakuachieni vizito viwili ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea
baada yangu, Quran na AhIul Bait wangu, viwili hivi havitaachana mpaka
vitakaponifikia katika Haudh.
"Tazama: Tafsir Ibn Kathir J.4 Uk. 122
Tafsirul Khazin J.1 Uk. 4
Tarikh Baghdad J.8 Uk. 442
Sahihi Muslim J.4 Uk. 1873
Sahihi Tirmidh J.2 Uk. 308
Jamiul Usul J.1 Uk. 187
AIbidayatu Wannihaya J.7 Uk. 362
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 163
Sahihi Muslim J.4 Uk. 1873
Sahihi Tirmidh J.2 Uk. 308
Jamiul Usul J.1 Uk. 187
AIbidayatu Wannihaya J.7 Uk. 362
Majmauz Zawaid J.9 Uk. 163
Hadithi hii inathibitisha kuwa baada ya kuondoka Mtume watakaoshika mahala
pake ni Ahlul Bait (a.s.) ambao tumekwisha waona katika tukio Ia
"KISAA" na katika tukio la "MUBAHALA" Mwenyezi Mungu
ameamrisha kufuata uongozi wao aliposema: "Shikamaneni na kamba ya
Mwenyezi Mungu nyote wala msitengane". (3:103). Tamko la kamba hapa ni
AHLUL BAIT".
Katika madhehebu yote ya kiislamu ni Shia ithnaashariyyah peke yake ndio
huwatawalisha Ahlulbayt. Madhehebu mengine huwasifia tu na tena kuna watu wao
ambao huwapa sifa zaidi hata ya sifa za Ahlulbayt.
Ninakukaribisheni watu wote katika kamba hii ya Mwenyezi ili nanyi muongoke
kama sisi Mashia.
Comments
Post a Comment