JINSI ABUBAKAR ALIVYOWAPINGA MASHAHIDI ILI KUHALALISHA DHULMA DHIDI YA AHLULBAYT.

JINSI ABUBAKAR ALIVYOWAPINGA MASHAHIDI ILI KUHALALISHA DHULMA DHIDI YA AHLULBAYT.

Hapa tunaongelea kesi aliyoifungua Fatuma bint Rasul (a.s) dhidi ya Abubakar ambaye ndiye aliyekuwa hakimu vilevile. Fatuma alikuwa anadai mali zake za mirathi ya baba yake ambazo Abubakar alizipora kwa madai kuwa mitume hawarithiwi. Sio mirathi Abubakar alipora hadi shamba ambalo Fatuma alikuwa amepewa na baba yake miaka miwili kabla ya kifo cha baba yake.

Kundi la kwanza la Mashahidi. Imam Ali, Hasani na Huseini (a.s). Abubakar akadai kuwa walikuwa mume na watoto, na  inawezekana wao kushawishiwa na maslahi binafsi.

Kumbuka kwamba Fatimah, Ali, Hasani na Huseini walikuwa watu pekee ambao walichaguliwa na Mtume kuthibitisha ukweli wake dhidi ya Wakristo wa Najrani - ambao walitakiwa waseme “Amin” kwa maombi ya Mtume ya kutaka laana ya Allah “dhidi  ya waongo.” Walikuwa ni watu pekee wanao ishi wakati huo  ambao walitakaswa na Allah kutokana na dhambi na makosa  yote. Na hakuna Mwislamu hata mmoja katika ulimwengu  ambaye anaweza kusema  kwamba wanaweza kusema uwongo.

Lakini Abu Bakar alikataa ushahidi wao kwa uwazi akisema  kwamba  ushahidi  wao ulishawishiwa na maslahi binafsi - kwa maneno mengine walikuwa waongo!!

Shahidi wa pili ni mke wa Abubakar mwenyewe yaani Asma bint Umais.
Abubakar akadai kuwa tatizo ni kuwa zamani alikuwa ameolewa na Ja’far, kaka yake Ali; na kwa hiyo, angeunga mkono madai ya Bani Hashim.  Alisahau kwamba alikuwa mke wake na hivyo ushahidi wake  dhidi ya maoni yake ulikuwa ni wa maana zaidi.

Na hata hivyo, je, lazima kwamba shahidi hapaswi kuwa rafiki wa upande wa yule ambaye anahudhuria (mbele ya mahakama) - kwamba ushahidi unaotolewa tu na adui ndio lazima ukubaliwe?

Shahidi wa tatu alikuwa Umm Ayman.
Abubakar akadai kuwa alikuwa sio Mwarabu na hakuweza kuongea  kiarabu fasaha. (Umm Ayman alikuwa msichana wa kitumwa wa Abdullah - baba yake Mtume). Mtume alimrithi, akamuozesha  kwa zayd bin Haritha, (na kwa mujibu wa Mtume alikuwa  miongoni mwa “watu wa Peponi”).

Je, ina maana kwamba ni watu tu wanao ongea kiarabu ndio  wanao weza kukubaliwa kama mashahidi? Au ni Waarabu tu  ndio wakweli na waaminifu? Hii ni ajabu ya mtu huyo aliyeamua kuchagua upotofu kuwa ndio imani yake.

Ukatili huu wa Khalifa ulizuia watu wengine kujitokeza mbele na kuota ushahidi kwa niaba ya Fatimah. Ikiwa Khalifa hana kusita kokote katika kumtweza na kumtukana Ali na watoto wake, vipi  watakuwa na uhakika kwamba heshima yao haitaharibiwa kama wakijitokeza kumuunga mkono Fatimah?

Madhumuni ya ushahidi ni kuthibitisha ukweli au vinginevyo wa  madai. Kama mtu ameridhishwa kwa ukweli wa madai, idadi ya mashahidi inakuwa ni ada tu, ambayo katika baadhi ya masuala ilitolewa hata na Abu Bakar mwenyewe. Mbona Jabir bin Abdallah Ansari,  Sahaba wa Mtume, alidai kwamba Mtume alimuahidi kiasi fulani  kutoka kwenye kodi ya Bahrain. Abu Bakar alikubali madai hayo  bila kutaka shahidi yeyote. Je huyo ndiye aliyekuwa mkweli kuliko familia ya Mtume?

Rejea
Fakhuruddin Ar-Razi, Tafsir Kabir, juzu ya 8, uk. 386.

Kanzu ’l-‘Ummal, juzu ya 3 uk.178-9

Comments