MAKHALIFA WA KIWAHABI HAWAKUJUA TAFSIR YA QUR’AN TAKATIFU

MAKHALIFA WA KIWAHABI HAWAKUJUA TAFSIR YA QUR’AN TAKATIFU.
Ni ajabu kuona kuwa watu waliojinyakulia ukhalifa kwa nguvu toka kwa Ahlulbayt na kudai kuwa ni makhalifa waongofu kumbe hawakujua hata tafsir ya Qur’an. Kwa mfano, Abubakar na Umar hawakuyafahamu mambo mengi miongoni mwa tafsiri ya (Qur'an) wala taawili yake, basi vipi itakuwa kwa wafuasi wao?

Na imethibiti katika athari ya kwamba Abubakr aliulizwa kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu isemayo: "Wafakihatan-Waabba" yaani, "Na matunda na malisho," basi Abubakr akasema: Ni mbingu gani itakayonifunika na ardhi gani itaniacha niketi humo endapo nitasema kuhusu kitabu cha Mwenyezi Mungu nisilolijua"?
Tazama: Al-Qastalani ndani ya Ir-shaad As-Sari Juz. 10 uk. 298
na ibn Hajar ndani ya Fat-h Al-Bari Juz. 13 uk. 230.

Kama ambavyo Umar bin Al-Khatab pia hakuifahamu maana hii.
Imepokewa toka kwa Anas bin Malik amesema, "Hakika Umar bin Al-Khatab alisoma akiwa juu ya Minbar (Faanbat-naa Fiha Habban Wainaban Waqadh-ban Wazaitunan Wanakhlan Wahadaiqa Ghul-ban Wafakihatan Waabba) Yaani, "Kisha tukaotesha humo (vyakula vilivyo) chembe chembe, na mizabibu na mboga, na mizeituni na mitende, na mabustani yenye miti iliyosongamana na matunda na malisho". (Qur'an 80: 27- 31)
Umar akasema: "Yote haya tunayajua, sasa hii Abban ni kitu gani? Kisha akasema: "Namuapa Mwenyezi Mungu hii ni takilifu (taabu) hulazimiki kufahamu nini Abban, fuateni yaliyobainishwa kwenu ndani ya kitabu, basi na muyatumie na yale msiyoyajua yategemezeeni kwa Mola wake".

Tazama:
Tafsiri ibn Jarir Juz. 3 uk. 38
Kanzul-Ummal Juz. 1 uk. 287,
Al-hakim ndani ya Mustadrak Juz. 2 uk: 14
Ad-Dhabi ndani ya Tal-Khis yake
Al-Khatib ndani ya Tarikh yake Juz. 11 uk. 468.


Ebu tuulizane endapo kama viongozi wa Uislamu hawakuijua vyema Qur’an na Sunnah za Mtume, Uislamu utakuwa na hali gani? Hii ndio sababu wafuasi wao hawaujui vyema Uislamu na wamegeuza fitna na ubabe kuwa ni Uislamu. Uislamu sahihi una himiza upole, unyenyekevu na kuamiliana vyema na watu wote bila duniani. 

Comments