MIRAJI (SAFARI YA MTUME
KWENDA MBINGUNI)
Jalaluddin Suyuti ameeleza
hadithi katika Tafsir Durr-e-Manthur
inatokana na Umar na Ibn Shuaib na ushuhuda wa Ibn Mardwaih inasema hivi: Mwaka mmoja kabla ya Hijra
(Mtume kuondoka Makka kwenda Madina) usiku wa mwezi kumi na saba (17)
Rabi-ul-Awwal, Mtume alipata heshima ya
kwenda Miraji. Abul Fida anaandika
kwamba zipo hitilafu za rai juu ya Miraji, kama amekwenda kwa kiwiliwili
chake au kama kuona ndoto ya kweli.
Watu kwa kawaida wanaamini
kwama Mtume alikwenda Miraji kwa kiwiliwili chake, lakini baadhi ya watu
wanadhani kwamba ilikuwa ndoto, lakini
ya kweli. Ndivyo ilivyoelezwa kwamba Aisha amesema Mtume hakwenda Miraji kwa kiwiliwili chake bali
Mola akafanya roho yake kwenda mbinguni
usiku wa Miraji. Vile vile imehadithiwa kuwa
i.
Muawiyah alikuwa akitakidi vivyo hivyo kwamba
Meraji ilikuwa usingizi wa kweli tu.
ii.
Ibn
Ishaq na Ibn Jarir al-Tabari vile vile wametoa hadithi kutokana kwa Aisha kwamba usiku wa Miraji
kiwiliwili cha Mtume kilikuwa pale pale
(kitandani) na Mwenyezi Mungu amepeleka roho yake tu juu mbinguni.
Lakini, Mulla Ali al-Qari
katika kitabu chake Sharh Fiqh-ul-Akbar anaandika kwamba kwenda Miraji Mtume
kwa kiwiliwili chake alipokuwa yu macho na kutembea juu huko mbinguni ni kweli
na yenye hakika na hadithi zinapokewa zinazothibitisha kisa cha Miraji.
Kwa hiyo kila mwenye
kukanusha au kutia shaka juu ya kwenda kwako Miraji basi huyo ni mkosi bali
mzushi.
Kadhalika Hafiz Abul Fazl
Ayadh al-Qadhi katika kitabu chake Ash-shifa bi Ta’rif Huquq al-Mustafa, ametia mkazo kwamba hakuna hitilafu yoyote
juu ya ukweli wa kwenda Mtume Miraji na
kama ilivyothibitisha Qur’ani. Akaendelea
zaidi kueleza kwamba Abul Hamra anasema kwamba Mtume amesema, “Usiku wa Miraji nilipopita kati ya
mbingu naliona juu ya ARSHI (mbingu ya mwisho juu) imeandikwa hivi: La Ilaha
Illallahu Muhammad ur-Rasool-ullah
Ayyaatohu be Aliyin”. (Hakika Mungu ni Yeye Subhanan Wataala tu na Muhammad ni
mjumbe (Rasul) wake, ambae nimemsaidiza (tegemeza na Ali)).
Vile vile Jalaluddin Suyuti
katika Durr-e-Manthur ameandika hadithi iliosemwa na Ibn Adi na Ibn Askari kama
walivyosikia kwa Sahaba Anas Ibn Malik kwamba Mtume alisema, “Nilipokwenda
Miraji nilishuhudia juu ya kipaa cha Arshi imeandikwa “La Ilaha Illallahu
Muhammad ur-Rasool-ullah Ayyaatohu be Aliyin”.
Comments
Post a Comment