BI AISHA AMPIGA VITA IMAM ALLY (a.s).

BI AISHA AMPIGA VITA IMAM ALLY (a.s).
Katika mwaka wa thelathini na sita Hijra, mama wa waumini, Bi Aisha alitoka nyumbani mwake Madina kwenda Basra ili kumpiga vita imam Ali bin Abi Talib (a.s.) na akafanya hivyo akiwa na kikosi cha watu elfu thalathini na ukamanda way eye mwenyewe, Twalha na Zubeir, katika vita viitwavyo vita vya Basra au vita vya Jamal. Vita hivi vilisababisha mauaji ya maelefu ya waislamu toka katika pande zote mbili.

Kitendo cha mke wa Mtume cha kutoka nyumbani mwake kwenda nje, ni jambo lililokatazwa na Mwenyeezi Mungu: "Na kaeni majumbani mwenu" 33:33, Mwana Aisha ameipuuza hukumu hii!

Aidha, kitendo cha kumpiga Imam Ali (a.s.) ni jambo linalomuweka mtu mahala pabaya. Imepokewa kutoka kwa A'diyyi bin Thabiti kutoka kwa Zuhry amesema: "Amesema Imam Ali kuwa: "Ninaapa kwa ambaye ameumba mbegu na akaumba upepo, hiyo ni ahadi ya Mtume kwangu mimi kuwa: Hanipendi mimi isipokuwa mu'umin na hanibughudhi (hanichukii) mimi isipokuwa mnafiki".
Rejea:
Sahihi-Muslim katika kitabul Iman
Sahihit Tirmidhi Juzu ya 2 Ukurasa wa 301
Musnad Ahmad Juzu ya 1 Ukurasa wa 84
Tarikh Baghdad Juzu ya 2 Ukurasa wa 255
Hilyatul Awliyaa Juzu ya 4 Ukurasa wa 185
Kanzul Ummal Juzu ya 6 Ukurasa wa 394
Mustadrakul Hakim Juzu ya 3 Ukurasa wa 129
Al Istiab Juzu ya 2 Ukurasa wa 214
Mwenyeezi Mungu anasema: "Haiwi kwa mwanamume aliyeamini, Mwenyeezi Mungu na Mtume wake wanapohukumu jambo wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyeezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotovu ulio wazi" 33:36.


Hiyo ndio hali halisi, jiulize kama hali iko hivi kwa kiongozi, itakuwaje kwa wanao ongozwa na mama huyu na baba yake? Ndugu zanguni walichokifanya Bi Aisha na baba yake si Uislamu kabisa. Uislamu ni upendo lakini upendo ungezidi zaidi pale ambapo Imam Ally ndiye aliyekuwa kipenzi wa Mtume kuliko wanaume wote wa zama zake. 

Comments