JE, ABUBAKAR KUFUATANA NA
MTUME NI FADHILA KWAKE?
Mwandishi wa historia
al-Mas’udi katika kitabu chake maarufu cha
historia kiitwacho Muruj adh-dhahab wa Ma’adin al-Jawahir anaandika kwamba Mtume alipohama Makka kwenda Madina,
Abu Bakr na watumwa wake Aamir bin Fahir na Abdalla bin Ariqat Daylani walifuatana naye. Abdalla Ibn Ariqat alikuwa
bado kusilimu bali walimchukuwa kuwaonyesha njia.
Abul Fida katika kitabu
chake Kitab al-Mukhtasar fi Akhbar-il-Bashar ameongeza kusema kwamba Mtume
alipoondoka Makka kuelekea Madina Maqureshi baada ya kumkosa nyumbani mwake
wakachukua hatua kubwa kumtafuta Mtume, basi Suraqa Ibn Malik alipelekwa
kumtafua Mtume, mara akafika karibu na Mtume, alipomwona tu Abu Bakr akasema,
“Eee Mtume, mwenye kututafuta amefika”. Mtume akajibu, “Usiogope na
usihuzunike; Mwenyezi Mungu yuko na sisi”.
Alipokwisha sema hayo Mtume
akamwapiza Suraqa. Mara tu farasi wa Suraqa akazama mpaka tumboni ndani ya
ardhi ngumu. Suraqa kwa moyo wa bidii akamwomba Mtume: “Niombee niepukane na
adhabu hii, na nakuahidi kwamba
nitawarejesha wote wanaokutafuta na
wenye kukufukuzia”.
Hapo Mtume akamwombea Dua na
Suraqa akatoka katika kuzama ardhini.
Pale pale akarejea na akawarejesha wale wote wanaomtafuta kila aliemkuta. Mtume
akafika Madina mwezi 12 Rabi-ul-Awwal mwaka wa kwanza wa Hijra na akateremka
Quba.
1. woga wa Abubakar tena mbele ya Mtume ni ushahidi kuwa hakuwa mcha Mungu wala jasiri
2. Angekuwa Imam Ally asingetikisika wala kubabaika mbele ya kafir Suraqa kama alivyotetemeka Abubakar.
3. Mtume alikuwa na uwezo usio wa kawaida na alifanya miujiza mingi iliyomshangaza kila Mtu.
Comments
Post a Comment