JE, MUAWIYA ALIKUWA AKILIPA
KISASI KWA WALIOMUUA UTHUMAN?
Muawiya aliutumia ujinga na
uchu wa pesa wa waislamu wa kipindi hicho kupata uungwaji mkono katika vita
vyake vya kuupokonya ukhalifa toka kwa Imam Ally (a.s).
Ibni Maghazli ameeleza
katika Manaqib yake ukurasa wa 128 "Dhikr Sifeen" kwamba: "Imam
'Ali aliandika barua kwa Muawiya akimwambia kwamba Maka na Madina wamekwisha
nipa kiapo cha utii mimi, ni lazima na wewe ufanye hivyo hivyo ili kuzuia vita
baina yetu yaani watu wa Iraq na Syria.
Mu'awiya alitumia kifo cha Uthman kuwa ni
sababu ya kukataa kuukubali ukhalifa wa Imam Ally (a.s) na kuwapotosha waarabu,
huku akiwahonga kwa fedha na ardhi ili wawe upande wake katika vita vyake vya
kugombea ukhalifa.
Ushahidi wa nia ya Mu'awiya
kuwa ni utawala na sio kulipiza kisasi kwa wauaji wa Uthuman, unapatikana toka
kwa mshirika wake wa karibu, yaani Amr
bin Aas.
Katika Ta'rikh Kamil mjaladi
wa 2 ukurasa wa 139, Amr bin Aas anasema kuwa kulipiza kisasi kifo cha Uthuman
ni mbinu na kisingizio tu, lakini nia yetu hasa ni utawala wa dunia hii;
Muawiya alipoyasikia haya akamkabidhi Misri iwe chini yake Amr kuonesha kuwa
alichokisema ni ukweli.
Hapa ndipo utauona wazi
unafiki wa Masunni. Sheikh wa Kisunni aitwaye Shah Abdul Aziz alitoa fatwa kuwa
kwa mujibu wa Ijma ya AhlulSunnah ni kuwa yeyote atakaye mpiga vita imam Ally
ni kafir (soma Hadiyyah Majeediyyah ukurasa wa 813).
Lakini kama walivyo masunni
wa kipindi hiki ambao hujichanganya kuwa upande wa Imam Ally na wakati huo huo
wanawapenda maadui zake, katika ukurasa huo huo aliandika maandiko ya kumlinda
Muawiyyah dhidi ya hukumu yao hiyo kwa madai kuwa Muawiyyah na watu wa Syria
walikuwa wakilipiza kisasi dhidi ya wauaji wa Uthuman.
Hii ni ajabu kuna watu wenye
elimu wanaweza kuungamkono vita vya kulipiza kisasi vilivyopiganwa dhidi ya
watu ambao hawakumuua Athuman. Labda watu wa Athuman watuambie kama aliyemuua
Athuman ni Imam Ally au wanae. Kama sio yeye hukumu ya kisasi inakujaje hapa? Kwa
nini wamtetee muuaji huyu wa waislamu.
Comments
Post a Comment