JINSI QUR’AN ILIVYOTILIA UMUHIMU SIRA au HISTORIA:

JINSI QUR’AN ILIVYOTILIA UMUHIMU SIRA au HISTORIA:

Hakika Qur’ani imetilia umuhimu sira kwa kubainisha sira ya manabii na watu wema. Ikataka tufuate sira yao na kujifunza kupitia sira ya wale waliopita huku tukiwaidhika na sira yao. Pia imetuhimiza kujali sira ya hitimisho la manabii na bwana wa mitume, Muhammad bin Abdullah (s.a.w.w.) ikataka tumuige3 baada ya kumwambia: “Na kwa hakika wewe unaongoza kwenye njia iliyonyooka.”4

3. Al-Ahzab: 21.
4. As-Shura: 52.

Kisha akawaamrisha waislamu wote kukazania yote yanayotoka kwa yule asiyetamka la matamanio yake akasema: “Na anachokupeni Mtume basi kipokeeni, na anachokukatazeni basi jiepusheni.”5

Kisha akatuelekeza kwa kizazi cha Mtume, ambao Mwenyezi Mungu kawaondolea uchafu na kuwatakasa kabisa6. Akahimiza kushikamana na wakweli na kufuata mwenendo wao, hivyo Mwenyezi Mungu akasema: “Enyi mlioamini, mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.”7

5. Al-Hashri: 7.
6. Al-Ahzab: 33.
7. At-Tawba: 119.


Ukimwona mtu anaogopa au hataki kusoma historia ya Uislamu na viongozi wake basi ujue huyo mtu hana mpango wa kuufuata Uislamu bali anayo njia yake nyingine anayoifuata, na anatumia Uislamu kwa maslahi yake mwenyewe. Ninakusudia kuwa maelezo anayoyatoa kuhusu Uislamu anayatoa kwa maadui wa Uislamu. 

Comments