MVINYO (POMBE) KABLA YA UISLAMU

MVINYO (POMBE) KABLA YA UISLAMU

Sayyid Ahmad Zayni Dahlan katika kitabu chake mashuhuri  alichokiandika juu ya maisha ya Mtume wetu (s.a.w.w.) kinachoitwa Siratun-Nabawiyah, anasema hivi: “wakati wa kufa kwake Abdul  Muttalib, akamuusia mwanawe Abu Talib juu ya Mtume wetu (s.a.w.w.), na vile vile kusema kwamba mvinyo ulikuwa haramu hata kabla Mtume hajatangaza dini ya Uislamu (katika zama za Jaahiliyyah).

Basi  alivyomwusia Abdul Muttalib mwanawe Abu Talib juu ya Mtume wetu (s.a.w.w.), akawa anampenda Mtume (s.a.w.w.) kuliko wanawe hadi wakati wa kulala (usiku) alimlaza ubavuni mwake, na alikuwa akimlisha chakula bora kabisa.”

Ikumbukwe kuwa Abu Talib alimlea Mtume Muhammad tokea akiwa mdogo kwa sababu yeye alikuwa mtoto yatima na hata babu yake alifariki akiwa bado mtoto.

Mtume Muhammad (s.a.w.w) alianza kufanya miujiza akiwa bado mdogo na mzee Abu Talib aliishuhudia miujiza yote na akawa anamtangaza kwa watu kuwa mtoto wake sio wa kawaida. Na pindi Mtume alipoanza rasmi kuutangaza Uislamu, mzee huyu aliukubali mara moja.
Hapa tunajifunza mambo matatu:
1.    Mvinyo ulikuwa haramu tokea zamani na wanaokunywa ni walafi na wanaokwenda kinyume na maelekezo ya Muumba.
2.    Mtume Muhammad (s.a.w.w) alijulikana kuwa ni Mtume tokea alipokuwa mtoto kutokana na tabia yake njema na miujiza aliyoifanya

3.    Abu Talib alikuwa mwislamu tena mkeleketwa hasa mpaka kifo chake.

Comments