SWALATUL - AAYAT

SWALATUL - AAYAT
 Sala ya Ayaat ni wajibu zama linapopatwa jua au mwezi, wakati wa mtetemeko na kimbunga na radi, na vizuko vingine vya mbinguni au ardhini.

Na namna ya kuswali kwake ni kama hivi:
1. Utanuwia, hali ya kuwa umesimama na umeelekea Qibla:  Naswali Salatul-Ayaat Rakaa mbili Qurbatan Ila llahi Taala.

2. Utasoma sura ya Al-Hamdu na sura nyingine, kisha utarukuu.

3. Utainuka kutoka katika rukuu; utasoma Al-Hamdu na sura nyingine, halafu utasoma Qunuti na utarukuu.

4. Utainuka kutoka rukuu. Na utasoma AI-Hamdu na sura, na utarukuu:

5. Utainuka kutoka rukuu, na utasoma Al-Hamdu na sura, halafu utasoma Qunut, na utarukuu.
6. Utainuka kutoka rukuu, na utasoma Al-Hamdu na sura, na utarukuu.

7. Utainuka kutoka rukuu, kisha utasujudu sijda mbili kisha utasimama kwa rakaa ya pili.

8. Utasoma Al-Hamdu na sura, na utasoma Qunut, halafu utarukuu.
9. Utainuka kutoka rukuu, utasoma Al-Hamdu na sura, na utarukuu.

10. Utainuka kutoka rukuu, utasoma Al-Hamdu na sura, na utasoma Qunuut, na utarukuu.

11. Utainuka kutoka rukuu, utasoma Al-Hamdu na sura, na utarukuu.

12. Utainuka kutoka rukuu, utasoma Al -Hamdu na sura, na utasoma Qunuut na utarukuu.

13. Baada ya hapo utainuka kutoka rukuu na kusujudu sijda mbili, na utasoma Tashaahhud na Salaam.



Itakuwa Sala ya Aayat ni rakaa mbili kwa Qunuut tano, na rukuu kumi, na sijda nne.

Comments