UFUFUO BAADA YA KIFO
Allah (s.w) anatwambia, “Wale ambao
wamekufuru walidai kuwa hawatafufuliwa, sema ndio, ninaapa kwa (haki ya) Mola
wangu, bila shaka mtafufuliwa kisha mtapewa habari za yale mliyo yafanya, na
jambo hilo ni jepesi kwa Mwenyezi Mungu”. “Suratu At-taghaabun aya ya 7”.
“Mwenyezi Mungu anakuhuisheni
kisha atakufisheni kisha atakukusanyeni siku ya kiama, hakuna shaka kuhusu
(suala) hilo”. “Suratul- Jaathiya”.
“Amesema kweli Mwenyezi Mungu
Mtukufu”.
Ndugu zangu nakuombeni tuwe makini
katika kuelewa dini yetu na kisha tuwe makini pia katika matendo yetu kwa
sababu yanarekodiwa, fanya ufanyayo ni lazima ufe na na kisha ufufuke na
kuhukumiwa. Tuogope sana hukumu ya mwisho kwa sababu siku hiyo itakuwa ni haki
tu.
Ni kweli kuwa sisi waislamu tunategemea
sana kuombewa na Mtume wetu na Ahlulbayt wake. Lakini utakapokuwa ni mtenda
mema utarahisisha kukubalika kwa uombezi wao na kinyume chake uombezi wao
unaweza kukataliwa na Allah (s.w). katika swala hili imani sahihi juu ya Allah,
Mtume na Ahlulbayt wake itakusaidia zaidi kuliko hata matendo yako. Tuwe makini
na imani zetu. Zingatia yafuatayo:
1. Hivi unamwamini Mwenyezi Mungu kwa usahihi (tawhid)
2. Je unampa Mtume sifa anayostahili
3. Je unawapenda na kuwatawalisha Ahlulbayt wa Mtume.
4. Je unawahurumia na kuwasaidia wanadamu na viumbe wengine
Kama majibu ya maswali haya yote ni
ndiyo, usiwe na hofu, tegemea kuwa utatetewa na Allah atakusamehe kwa sababu
yeye ni msamehevu tena mwenye huruma.
Comments
Post a Comment