UIMAMU NI NGUZO MUHIMU KATIKA UISLAMU
Mwenyezi mungu anasema:
(Ewe mwanadamu!
Ikumbuke) siku Tutakapowaita kila watu pamoja na Imamu wao; basi atakayepewa
kitabu (chake cha Amali) kwa mkono wa kulia, hao watavisoma vitabu vyao (kwa
furaha); ... (Bani Isra’il, 17:71)
mtukufu mtume (s.a.w.w.) amesema: “Yeyote yule afaye pasi na
kumjua Imamu wa zama zake, atakuwa kafa kifo cha ujinga”.
MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.) AMESEMA:
“Hao (Ulul Amr watajwao mwenye Qur’ani 4:59) ni Makhalifa wangu na Maimamu
wa Waislamu baada yangu. Wa kwanza ni Ali, kisha ni Hassan, kisha ni Husayn,
kisha ni Ali bin Husayn, kisha ni Muhammad bin Ali, kisha ni Jafar bin
Muhammad, kisha ni Musa bin Jafar, kisha ni Ali bin Musa, kisha ni Muhammad bin
Ali, kisha ni Ali bin Muhammad, kisha ni Hassan bin Ali, kisha ni Muhammad bin
Hassan (Mahdi)..”.
(“Kifayatul Athar” na rawdhatul ahbab, vya Hafidh
Jamaluddin Muhaddith).
MASWALI KWAKO:
1. Imam wa zama zako anaitwa nani?
2. Kama Mtume anasema makhalifa ni 12 na
amewataja kwa majina, je wewe unawafuata makhalifa hao?
3. Katika makhalifa waliotajwa na Mtume:
majina ya Abubakar, Umar na Uthman hayamo. Unasema Mtume alikosea au wewe ndiwe
uliyekosea kwa kuwafuata watu waliokuwa hawakuteuliwa na Mtume?
Comments
Post a Comment